Uchaguzi Zimbabwe: Maduka yafungwa Harare huku jeshi likipiga doria

Bwana Chamisa alisema siku ya Jumatatu kwamba uchaguzi huo wa Jumamosi ulifanyiwa udanganyifu ili kumpatia rais Mnangagwa ushindi.
Uchaguzi huo ulikuwa wa kwanza tangu kiongozi wa muda mrefu Robert Mugabe kung'atuliwa madarakani.Biashara zimefungwa katika mji mkuu wa Zimbabwe harare huku taifa hilo likisubiri kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi yanayozozaniwa.
Matumizi ya nguvu ya serikali dhidi ya upinzani nchini Zibabwe baada ya uchaguzi wa Jumatatu yameichochea jamii ya kimataifa kutoa wito wa kumaliza vurugu.
Umoja wa mataifa na umoja wa ulaya kwa pamoja wamekemea juu vurugu zilizotokea na polisi kufyatua risasi kwa waandamanaji.
Uchaguzi Zimbabwe: Maduka yafungwa Harare huku jeshi likipiga doria
Reviewed by RICH VOICE
on
Agosti 02, 2018
Rating:
Hakuna maoni