Queen Darleen amshauri Harmonize



First Lady kutoka Label ya WCB, Queen Darleen ametoa ushauri mzito kwa Harmonize kuhusu maisha yake ya kimuziki na mahusiano.

Muimbaji huyo amemshari Harmonize kutokata tamaa na muziki wake ingawa watu wa kumkatisha tamaa wapo, huku akimsisitiza kuwa kuepeka kuwa katika mahusiano na wanawake wengi.
“Apunguze uhuni, atulie, mtoto wa watu masikini ya Mungu, Mzungu (Sarah) anampenda, yeye muhuni. Mdogo wangu maisha ya uhuni siyo mazuri, unakuwa kama mfalme Sulemani, ache hizo,” Queen Darleen ameiambia Radio Five.
Harmonize na Queen Darleen wameshakutana katika ngoma inayokwenda kwa jina la Zilipendwa ambayo ilikutanisha wasanii kama Diamond, Lava Lava, Rayvanny, Rich Mavoko na Mbosso.

Queen Darleen amshauri Harmonize Queen Darleen amshauri Harmonize Reviewed by RICH VOICE on Mei 04, 2018 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...