Friday, November 11, 2016


Picha: Rais Magufuli Alipomtembelea na Kumjulia Hali Mke wake na Wagonjwa wengine Waliolazwa Muhimbili


Mke wa Rais wa Tanzania John Magufuli, Janeth, amelazwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili. Jana  Ikulu imetoa picha ya Rais Magufuli akimjulia hali katika wodi ya Sewa Haji.

Taarifa ya ikulu ilisema , alipokuwa anamjulia hali mkewe, pamoja na  balozi na waziri mstaafu wa Tanzania Omar Ramadhan Mapuri, wagonjwa waliolazwa katika wodi ya Sewa Haji walimshukuru kwa hatua zilizochukuliwa na serikali kuboresha hospitali ya taifa ya Muhimbili

Pia walisema kuwa licha ya kuboreshwa kwa mazingira ya hospitali, wanapata huduma nzuri kutoka kwa madaktari na wauguzi.
Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongea na mkewe Mama Janeth Magufuli ambaye amelazwa kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam akipatiwa matibabu jana Novemba 10, 2016. Kulia ni Dkt Edward Ngwale akiwa na wauguzi katika wodi hiyo.
Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimjulia hali Waziri wa Zamani Balozi Omar Ramadhani Mapuri ambaye amelazwa kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam akipatiwa matibabu jana Novemba 10, 2016.
Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwashukuru na kuwapongeza kwa kazi nzuri baadhi ya madaktari na wauguzi kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam alipotembelea wagonjwa pamoja na mkewe ambaye anapatiwa matibabu jana Novemba 10, 2016.
Rais wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwafariji baadhi ya wagonjwa kwenye wodi ya Sewa Haji katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam alipotembelea kuona wagonjwa pamoja na mkewe ambaye anapatiwa matibabu hapo jana Novemba 10, 2016.

 

Friday, November 11, 2016


Wizara Ya Mambo Ya Ndani Ya Nchi Yakamilisha Rasmi Taratibu Za Ajira Za Uhamiaji Kwa Ngazi Ya Askari Na Maafisa


 

 

 

Friday, November 11, 2016


Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya Novemba 11



Friday, November 11, 2016


Wizara Ya Mambo Ya Ndani Ya Nchi Yakamilisha Rasmi Taratibu Za Ajira Za Uhamiaji Kwa Ngazi Ya Askari Na Maafisa


Reviewed by RICH VOICE on Novemba 11, 2016 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...