FRIDAY 09/09/2016

 LEO TUNAANZA NA MICHEZO 

STRAIKA WA CHELSEA ARUDISHWA SIKU 9 TU TOKA UHAMISHONI!

и
CHELSEA-REMYLoic Remy amerejeshwa Klabuni kwake Chelsea Siku 9 tu baada ya kuwa kwa Mkopo huko Crystal Palace bila kucheza hata Mechi moja baada ya kuumia.
Reny, Raia wa Ufaransa mwenye Miaka 29, aliumia Pajani Mazoezini Majuzi Jumatatu na sasa amerejeshwa Klabuni kwake Chelsea kupata matibabu zaidi.
Palace imethibitisha tukio hili na kusema atakuwa nje kwa Wiki kadhaa.
Meneja wa Palace, Alan Pardew, amesema: “Kwa bahati mbaya Remy aliumia Mazoezini Jumatatu. Si vibaya sana lakini Wikiendi hii hawezi kucheza na sijui atakuwa nje kwa muda gani hadi vipimo vikamilike.”
Remy alijiunga na Chelsea Mwaka 2014 na kufunga Bao 8 katika Mechi 32.
Hadi sasa Palace wamecheza Mechi 3 za Ligi Kuu England na kuambua Pointi 1 tu na Jumamosi wapo Ugenini kucheza na Middlesbrough.
Mapema Leo Palace walimsaini Kiungo wa zamani wa Arsenal Mathieu Flamini ambae ni Mchezaji Huru na kufikisha idadi ya Wachezaji wao wapya kwa Msimu huu kuwa Watano na wengine ni Andros Townsend, Steve Mandanda, James Tomkins, Christian Benteke na huyu Loic Remy.
LIGI KUU ENGLAND
Ratiba:
**Saa za Bongo
Jumamosi Septemba 10
1430 Man United v Man City                
1700 Arsenal v Southampton                
1700 Bournemouth v West Brom           
1700 Burnley v Hull          
1700 Middlesbrough v Crystal Palace               
1700 Stoke v Tottenham             
1700 West Ham v Watford          
1930 Liverpool v Leicester          
Jumapili Septemba 11
1800 Swansea v Chelsea   
Jumatatu Septemba 12
2200 Sunderland v Everton     

ANFIELD ‘MPYA - JUMAMOSI LIVERPOOL KUIFUNGUA NA MABINGWA LEICESTER!


ANFIELD-JUKWAAKUU-JIPYALIVERPOOL watacheza Uwanja wa Nyumbani kwao Anfield Jumamosi kwa mara ya kwanza Msimu huu baada kucheza Mechi 3 za Ligi Kuu England, EPL, Ugenini wakipisha upanuzi wa Jukwaa Kuu la Uwanja wao.
Jumamosi Liverpool watawakaribisha Mabingwa Watetezi wa England Leicester City kwenye Mechi ya EPL ambayo itatanguliwa na Ufunguzi rasmi wa Jukwaa Kuu jipya ambao Mmiliki Mkuu wa Klabu hiyo kutoka Kampuni ya Kimarekani Fenway Group, John W Henry, Mwenyekiti Tom Werner na Rais Mike Gordon watahudhuria.
+++++++++++++++++++++++
JE WAJUA?
-Kupanuliwa kwa Jukwaa Kuu la Anfield kutaiongezea Mapato Liverpool kwa Siku za Mechi kwa kiwango cha Pauni Milioni 20 hadi 30 kwa Msimu.
-Kabla, Liverpool walikuwa wakivuna Pauni Milioni 59 tu.
-Manchester United ndio wanaovuna kiwango cha juu kabisa cha zaidi ya Pauni Milioni 100.
+++++++++++++++++++++++
Jukwaa hilo limepanuliwa na kuongezwa Ngazi 3 juu za kukalia Washabiki, kupanua Ukumbi wa Wachezaji kuingia na kutoka Uwanjani kutoka Vyumba vya Kubadili Jezi, Mabenchi ya Wachezaji wa Akiba na Jopo lao la Ufundi kutengenezwa upya, sehemu maalum kwa Walemavu na kuboreshwa kwa miundo mbinu ya Watazamaji.
Jukwaa Kuu la Anfield litaongeza Viti 8,500 na kuufanya Uwanja huo sasa upakie Watazamaji 54,000.
LIGI KUU ENGLAND
Ratiba:
**Saa za Bongo
Jumamosi Septemba 10
1430 Man United v Man City                
1700 Arsenal v Southampton                
1700 Bournemouth v West Brom           
1700 Burnley v Hull          
1700 Middlesbrough v Crystal Palace               
1700 Stoke v Tottenham             
1700 West Ham v Watford          
1930 Liverpool v Leicester          
Jumapili Septemba 11
1800 Swansea v Chelsea   
Jumatatu Septemba 12
2200 Sunderland v Everton  

KUELEKEA DABI YA MANCHESTER: MOURINHO ANENA UPINZANI WAKE NA GUARDIOLA!

>>”LIGI KUU ENGLAND SI LA LIGA YENYE SAMAKI MKUBWA MMOJA TU, HUKU KUNA PAPA KILA KONA!”
MOU-PEPWAKATI Dunia ya Soka ikisubiri kwa hamu Dabi ya Manchester itakayochezwa Jumamosi hii Uwanjani Old Trafford kati ya Mahasimu Manchester United na Manchester United huku kukiwa na shauku ya ziada ya kuwaona Mameneja wapya wa Klabu hizo, Jose Mourinho na Pep Guardiola, wakikwaana kwa mara nyingine, Mourinho ametoa tahadhari kubwa.
Mourinho, ambae sasa ni Meneja wa Man United, ameonya hatatumbukizwa tena kwenye uhasama wa kupindukia na Guardiola ambae ni Meneja wa Man City.
Wawili hao walikuwa na upinzani uliojaa vituko na bashasha kubwa huko Spain walipoongoza Timu pinzani wakati Mourinho akiwa Real na Guardiola akiwa Barcelona.
Lakini, kabla ya wote kuwa Makocha Viongozi, Wawili hao walikuwa Timu moja Barcelona, Mourinho akiwa mmoja wa Jopo la Makocha na Guardiola akiwa Mchezaji na kisha kuanza Ukocha.
Wanahabari na Wachambuzi huko Uingereza, na Duniani kote, wamekuwa wakingoja kwa shauku Wawili hao wakikutana uso kwa uso kwa mara ya kwanza huko England.
Lakini Mourinho amesema kwenye La Liga wasiwasi wake mkubwa ulikuwa kwa Samaki mmoja mkubwa tu lakini England kuna Papa kila kona.
Ameeleza: “Uzoefu wangu hauniruhusu niwe mpumbavu. Kwa Miaka Miwili mimi na Pep tulikuwa kwenye Ligi ambayo Bingwa nakuwa mimi au yeye, Real Madrid au Barcelona!”
“Kwa hali kama hiyo, kukwaruzana kibinafsi kunaeleweka kwani huweza kubadilisha mambo!”
“Lakini kwenye Ligi Kuu, nikimtilia mkazo yeye na Manchester City, na yeye atie mkazo kwangu na Manchester United, Mtu mwingine atakuwa Bingwa!”

ZA KIMATAIFAAAA

Matumizi ya Koili ni bora kuliko tembe katika kuzuia ujauzito


Wanawake wanapaswa kushauriwa kwamba njia ya kuzuia ujauzito ya matumizi ya koili ni bora zaidi kuliko njia ya dharura ya kumeza vidonge vinavyomezwa baada ya tendo la ngono (morning-after pill), kwa mujibu wa ushauri mpya uliotolewa Uingereza
Limekuwa likishauriwa ni "jambo jema " kuwapatia wanawake coili kwa kipindi cha muongo.
Lakini Taasisi ya Kitaifa ya Uingereza ya afya na ubora wa Kliniki (NICE) inasema ushauri kuhusu suala hili unapaswa kuboreshwa.
Kati ya mwaka 2014 na 2015, 95% ya wanawale waliopewa vidonge vya dharura na huduma za afya na masuala ya ngono kwa ujumla walipewa vidonge vya kuzuia mimba vya... morning-after pill.
Coil, ambayo pia hutambuliwa kwa lugha ya kitaalam kama...intrauterine device au IUD, ni njia inayofaa ikiwa itaingizwa katika siku tano baada ya kufanya ngono bila kinga na Coil lazima zipachikwe vizuri hasa na daktari ama muunuzi aliyepewa mafunzo, katika kliniki ya afya ya uzazi ama kwenye kituo cha upasuaji.
Kama itakuwa vigumu kumpata daktari katika muda wa siku tano , mwanamke anaweza kushauriwa kumeza tembe za morning-after pill kabla ya coili haijafungwa.
'Kufahamu muda ni muhimu'
Sue Burchill, mkuu wa wauguzi katika hospitali ya Brook, ambayo hutoa huduma za afya ya ngono kwa vijana 25,000 walio chini ya umri wa mika 25 kila mwaka anasema, said: "runaamini vijana wote wanapaswa kuwa na taarifa sahihi kuhusu njia tofauti za dharura za kuzuia mimba zilizopo ili wawe na uelewa kuhusu uamuzi juu ya njia iliyo bora kwa mahitaji ya binafsi, na tunatolea witro mamlaka za ndani husika nchini kutopuuza hili kwa kupunguza udhamini kwa ajili ya huduma za afya ya ngono
"tunafahamu kwamba matumizi ya coili ndio njia iliyo inayofaa ya uziaji mimba wa dharura iliyopo, kwa hivyo tunapaswa kuendelea kuhakikisha tunawezesha watu kutumia injia hii na kuimarisha utaoaji wa huduma hizi miongoni mwa wale wanaozitoa."
Profesa Gillian Leng, naibu mkurugenzi mkuu wa NICE, anasema : "kwa kweli ni muhimu kwamba huduma zote za kuziwia mimba zitolewe kwa wanawake zikiambatana na ushauri mzuri kuhusu njia za kuzuia mimba.
" Pia tunataka kuhakikisha wanawake wanaelezwa kwamba coili ni njia bora zaidi ya kuzuwia mimba kuliko tembe katika wakati wa dharura."
DK Jan Wake, wa GP na mjumbe wa shirika linalotoa maagizo kuhusu njia za kupanga uzazi, anasema : "kuelewa muda wa tendo la ngono, hata hivyo, ni muhimu na wanawake wanaoamua kutumia coili wanapaswa kutembelea kliniki walizoshauriwa kwenda mapema iwezekanavyo.

Watalii 45 wakwama mlimani Ufaransa

Juhudi za uokoaji za kuwanasua watalii 45 ambao wamekwama kwenye magari ya kutumia kamba katika mlima wa Mont Blanc, Ufaransa zimeanza tena.
Watalii hao walilala usiku wa Alhamisi kwenye kibaridi kikali wakiwa wamekwama juu ya barafu takriban 3,800m (futi 12,468) juu mlimani.
Walikuwa miongoni mwa watu 110 waliokwama baada ya magari hayo kupatwa na hitilafu Alhamisi alasiri.
Inaaminika magari hayo yalikwama baada ya kamba kushikana kutokana na upepo mkali.
Watu 65 waliokolwa kwa kutuia helikopta baadaye Alhamisi lakini juhudi zikasitishwa giza lilipoingia na kukawa na mawingu hivyo kuifanya vigumu kuona.
"Tulilazimika kusitisha juhudi za uokoaji kwa sababu za kiusalama," alisema Georges Francois Leclerc, mkuu wa idara ya uokoaji ya Haute-Savoie.
"Tunatumai tutawapata wote salama Ijumaa asubuhi," alisema ni kuongeza kwamba ni operesheni ngumu sana.
Watalii waliokwama walipewa vyakula, blanketi na maji.

Maji ya mto yageuka 'rangi ya damu' Urusi

Wachunguzi wa masuala ya mazingira nchini Urusi wanajaribu kubaini chanzo cha maji ya mto ulio karibu na kiwanda cha nikeli cha kampuni ya Norilsk Nickel yamebadilika rangi na kwua na rangi nyekundu.
Picha za maji ya mto Daldykan ambayo yamebadilika rangi zimesambazwa sana katika vyombo vya habari Urusi.
Gazeti la serikali la Rossiiskaya Gazeta linasema kuvuja kwa bomba la kusafirisha taka za mchanganyiko wa shaba nyekundu na nikeli huenda likawa kiini cha maji hayo kubadilika rangi.
Norilsk Nickel ndiyo mzalishaji mkubwa zaidi wa nikeli na palladium duniani.

Kampuni hiyo ina vinu na tanuri nyingi rasi ya Taimyr eneo la Krasnoyarsk katika jimbo la Siberia. Ujenzi wa vinu hivyo vikubwa ulifanyika enzi za muungano wa Usovieti.
Kampuni hiyo ina kiwanda kwa jina Nadezhda karibu na mto Daldykan lakini maafisa wake wanasema hawajapata dalili zozote za uchafuzi kutoka kwa kiwanda hicho.
Rais wa kampuni hiyo ni bilionea Vladimir Potanin.

 

Korea Kaskazini yalipua bomu ‘sawa na la Hiroshima’

Shirika la habari la serikali ya Korea Kaskazini limesema taifa hilo limefanya majaribio ya bomu kupima uwezo wa bomu lake la nyuklia la kurushwa kwa kombora.
Mlipuko wa bomu hilo umesababisha tetemeko la ardhi katika eneo lililofanyiwa majaribio.
Tetemeko hilo lilikuwa na nguvu ya 5.3 kwenye vipimo vya Richter.
Maafisa wa jeshi la Korea Kusini wanakadiria kwamba mlipuko huo ulikuwa sawa na wa kilo tani kumi za TNT, ukubwa sawa na wa bomu lililoangushwa Hiroshima na Marekani wakati wa vita vikuu vya pili vya dunia. Baadhi wanasema huenda bomu hilo la Korea Kaskazini likawa lilikuwa na nguvu ya kilo tani 20.
Bomu lililoangushwa Hiroshima mwaka 1945 lilikuwa na nguvu ya kilo tani 15 (tani 15,000).
Bomu lenye nguvu zaidi la nyuklia lililowahi kulipuliwa lilikuwa lile lililopewa jina Tsar-bomba, ambalo lililipuliwa na Urusi mwaka 1961.

Lilikuwa na nguvu ya mega tani 50, sawa na nguvu ya tani milioni 50 za TNT (50,000,000).
Wataalamu bado wanaendelea kudadisi iwapo lilikuwa bomu la haidrojeni, jambo ambalo linaweza kulipa nguvu zaidi kushinda mlipuko wa bomu la kawaida la nyuklia.
Hilo likithibitishwa, basi itakuwa ni mara ya tano kwa Pyongyang kutekeleza jaribio la silaha za kinyuklia.
Jaribio la leo limetekelezwa siku ambayo serikali inaadhimisha kuanzishwa kwa taifa la sasa la Korea Kaskazini mwaka 1948.
Jamii ya kimataifa imeghadhabishwa na hatua hiyo ya Korea Kaskazini.
Image copyright Reuters
Image caption Rais Kim Jong-un ameonyeshwa kwenye runinga akiwa amejaa tabasamu
Rais wa Korea Kusini Park Geun-hye ametaja jaribio hilo kuwa "jaribio la kujiangamiza" ambalo linaonyesha "kutomakinika" kwa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un.
Bi Park, ambaye amesitisha ghafla ziara yake ng'ambo, amesema baada ya kutekeleza jaribio hilo la tano la nyuklia "serikali ya Kim Jong-un itakaribisha vikwazo zaidi na kutengwa zaidi na jamii ya kimataifa."

"Uchokozi kama huu utaongeza kazi safari yake ya kuelekea kwenye maangamizi."
Bi Park alifanya pia amzungumzo ya dharura na Rais wa Marekani Barack Obama kwa njia ya simu.

Kuvumiliwa

China, mshirika mkuu wa Korea Kaskazini kidiplomasia, pia imeshutumu hatua hiyo na kuihimiza Pyongyang kukoma kuchukua hatua ambazo zinaweza kuzidisha hali.
Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe, amesema majaribio kama hayo ya Korea Kaskazini hayawezi kuvumiliwa.

 

Friday, September 9, 2016

Viongozi wa Afrika Mashariki Waigomea Ulaya....Wajipa Miezi Mitatu Kuutafakari Mkataba wa EPA


SeeBait

JUMUIYA ya Afrika Mashariki (EAC), imeiomba Jumuiya ya Ulaya (EU), iipe muda wa miezi mitatu kujua hatima ya wao kusaini Mkataba wa Kiuchumi na Jumuia hiyo (EPA).

Uamuzi huo ulifikiwa jana Ikulu Dar es Salaam na viongozi wa Jumuiya hiyo baada ya kikao cha 17 kilichodumu kwa takribani saa sita.

Akizungumza baada ya kikao hicho, Mwenyekiti wa EAC, Rais John Magufuli alisema kikao hicho kilikuwa na ajenda nne, ila ya EPA ilikuwa ngumu kulingana na uzito wake.

Alitaja ajenda hizo kuwa ni ripoti ya mgogoro wa Burundi, kuingizwa rasmi kwa Sudan Kusini kwene Jumuiya, kupitishwa kwa Naibu Katibu Mkuu wa EAC na EPA.

Rais Magufuli alisema viongozi wote kwa pamoja walikubaliana kupewa muda wa miezi mitatu ili Sekretarieti ya EAC iangalie na kupitia masharti ya EPA kabla ya kusaini ili kila mmoja afaidike.

Hata hivyo nchi ambazo zilishasaini makubaliano hayo kutoka Jumuiya hiyo ni Kenya.

Alisema katika kikao hicho, walibaini mambo 10 ambayo yanapaswa kuangaliwa kabla ya kufikia uamuzi kwa maslahi ya nchi na wananchi.

Mwenyekiti alitaja mambo ya kuangaliwa kuwa ni kwa namna gani nchi za EAC zitafaidika, njia gani itatumika kuzuia bidhaa za kilimo na kulinda wakulima.

Maeneo mengine ni usawa, makusanyo yatokanayo na bidhaa zitakazoingizwa, Burundi itasainije huku ikiwa imewekewa vikwazo na EU, kujitoa kwa Uingereza EU na athari zake, kukosekana kipengele cha kuruhusu nchi zingine kujihusisha na nchi za EAC kibiashara, kukosekana ushuru wa forodha na kipengele cha nchi kujitoa pale inapoona haijaridhika na mkataba.

Rais Magufuli alisema mkataba huo ukisainiwa kwa wakati huu, nchi wanachama zinaweza kuingia kwenye mtego mbaya.

“Tumejadiliana kwa muda mrefu ila mjadala mkubwa ulikuwa suala la EPA ambapo tumekubaliana tupewe miezi mitatu ili tukutane Januari na kutoa uamuzi wa pamoja,” alisema Magufuli.

Alisema Tanzania iko kwenye mkakati wa kujenga viwanda, hivyo ni lazima iwe makini katika kusaini mkataba huo.

Aidha, aliiomba EU kutoiadhibu Kenya kutokana na uamuzi huo kwani nia yao ni nzuri hivyo wapewe nafasi.

Mwenyekiti huyo alisema viongozi wote walikubaliana kuiidhinisha Sudani Kusini kuwa mwanachama wa EAC na Christopher Bazivamo kutoka Rwanda kuwa Naibu Katibu Mkuu Mpya na mapendekezo ya kutatua mgogoro wa Burundi.

 

 

 

Friday, September 9, 2016

Makamu Wa Rais Atembelea Kituo Cha Kuchakata Gesi .....awataka wafanyakazi kufanya kazi kwa uzalendo


SeeBait

Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amewataka wafanyakazi wa kiwanda cha kuchakata gesi asilia kilichopo Madimba mkoani Mtwara wawe wazalendo na wafanye kazi kwa bidii katika kulinda na kuutunza uwekezaji huo mkubwa ambao serikali inautegemea katika uzalishaji wa nishati ya umeme wakati taifa linaelekea kwenye nchi ya viwanda.

Makamu wa Rais ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wafanyakazi na watendaji wa kiwanda hicho baada ya kutembelea kiwanda kwa mara ya kwanza tangu ashike wadhifa huo kwa lengo la kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa kiwandani hapo akiwa katika ziara yake ya kikazi ya siku nne mkoani Mtwara.

Amesema kiwanda cha kuchakata gesi asilia ni hazina kubwa  kwa Taifa hivyo ni kikalindwa na kutunzwa ipasavyo kutokana na umuhimu wake katika uzalishaji wa nishati ya umeme kwa maendeleo ya nchi.

Makamu wa Rais pia amewashukuru na kuwapongeza wafanyakazi wa kiwanda hicho cha kuchakata gesi asilia cha Madimba na amewahakikishia kuwa serikali itaendelea kuwajali na kuwathamini katika utendaji wao wa kazi na kwamba serikali itahakikisha wafanyakazi wa kiwanda hicho wanapewa motisha ya kutosha ili waongeze maradufu utendaji wao wa kazi ili malengo ya serikali ya kuleta maendeleo kwa wananchi kupitia viwanda inatimia kwa sababu taifa litakuwa na nishati ya umeme ya uhakika.

Makamu wa Rais amewataka watendaji wa Shirika la Maendeleo la Petroli (TPDC) ambalo linasimamia mradi huo kuhakikisha wanatenga fedha kwa ajili ya kusaidia huduma za jamii katika vijiji vinavyozunguka mradi huo kila mwaka ili wananchi waweze kuwa walinzi wa mitambo hiyo.

Akitoa maelezo mafupi ya mradi huo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. James Mdoe amesema kiwanda hicho kina uwezo wa kuchakata gesi ya futi za ujazo milioni 210 kwa siku.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Kiwanda cha kuchakata gesi cha Madimba Mhandisi Leonce namna gesi inavyopokelewa na kuchakatwa na kusafirishwa kwa watumiaji.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan akiangalia mfumo wa uendeshaji na usalama wa kiwanda cha kuchakata gesi cha Madimba mkoani Mtwara.

 

Friday, September 9, 2016

Profesa Semboja adai Ukubwa wa deni la taifa hauwezi kuyumbisha uchumi


SeeBait


Na: Frank Shija, MAELEZO
Ukubwa wa deni la taifa siyo jambo linaloweza kusababisha kuyumba kwa uchumi wa nchi, kinachooneka ni kuendela kuaminiwa kwa Tanzania ndani na nje ya nchi jambo linalopelekea tuna pata fursa ya kukopesheka kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Hayo yamebainishwa na Mchambuzi wa masuala ya kiuchumi, Profesa Haji Semboja alipofanya mahojiano maalum na mwandishi kutoka Idara ya Habari, MAELEZO kuhusu hali ya uchumi ilivyo kutokana na ongezeko la deni la Taifa leo Jijini Dar es Salaam.

“Ukubwa wa deni la taifa siyo mzigo mbaya, ni mzigo wa kimaendeleo. Unnecessary devil” Alisema Profesa Semboja.

Aliongeza kuwa kutokana kwa imani waliyo nayo wahisani ndani na nje ya nchi ndiyo maana washirika wetu wanatukopesha fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo kama ambavyo tumeshuhudia ujenzi wa Daraja la Kigamboni, hivi karibuni tutanufaika na usafiri wa ndege”. Alisema Profesa Semboja.

Aidha amempongeza Rais wa Awamu ya Tano Mhe. Dkt. Jonh Pombe Joseph Magufuli kwa hatua alizochukua za kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma kwa kuondoa safari za nje zisizo za rasmi pamoja na kupiga vita vitendo vya rushwa.

Semboja aliendelea kusema kuwa kinachofanyika hivi sasa ni Serikali ya awamu ya Tano kulipa madeni ya watangulizi wake huku ikitekeleza miradi ya maendeleo jambo linaloongeza imani miongoni mwa wahisani.

Hata hivyo alionya juu ya matumizi mabaya ya rasilimali fedha kuwa zinasababisha kushindwa kutekeleza wajibu wa kulipa deni kwa wakati na kupelekea kulimbikiza madeni jambo ambalo si sahihi.

Alitajaa baadhi ya matumizi mabaya ya fedha kuwa ni pamoja na safari za nje na ndani ya nchi zisizokuwa na tija, ulevi, kupelekea fedha katika miradi isiyopangwa na mengine.

Wananchi wametakiwa kutoyumbishwa na waelewi kuwa kupitia fedha zinazokopwa wanufaika wakuu ni wananchi wenyewe, mfano fedha zitakazo tumika kujenga Nyumba za Magomeni ambazo Mhe. Rais amehaidi waliokuwa wakazi wake kuishi bila kulipia kwa kipindi cha miaka mitano zikitokana na mikopo hiyo wananufaika.

 

Friday, September 9, 2016

Msafara wa Makamu wa Rais, Samia Suluhu wapata ajali Mtwara.


SeeBait

Msafara wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama Samia Suluhu Hassan ambao ulikuwa unaelekea Wilayani Tandahimba ukitokea Ikulu ndogo ya Rais ,mkoani Mtwara, umepata ajali na kusababisha majeruhi ambao wamekimbizwa hospitali ya rufaa Ligula.

Ajali imetokea mbele kidogo ya kijiji cha Nanguruwe kilichopo halmashauri ya wilaya ya Mtwara .Majeruhi walioumia ni dereva  pamoja na wasaidizi wanne wa Makamu wa Rais.
 
Awali kabla ya gari hilo lililobeba wasaidizi wa Makamu wa Rais kuacha njia na kupinduka, gari liliokuwa limebeba waandishi wa habari wa channel ten, startv na clouds tv liliacha njia na nusura kupinduka.

Barabara ya kutoka Mtwara kuelekea Tandahimba si ya kiwango cha kuridhisha na kuruhusu magari kwenda mwendokasi hali iliyosababisha magari hayo kuacha njia na moja kupinduka kabisa na kusababisha majeruhi.

 

 

Friday, September 9, 2016

Mahakama Yaizuia NHC Kupiga Mnada Mali za Freeman Mbowe


SeeBait

Mahakama Kuu ya Tanzania, Kitengo cha Ardhi imeliamuru Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kutouza au kupiga mnada mali za Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), mpaka kesi ya msingi itakapomalizika.

Shirika hilo lilizichukua mali mbalimbali za kampuni za Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Hai, wiki iliyopita kupitia mawakala wa kampuni ya Fosters Auctioneers katika jengo lililopo makutano ya mitaa ya Mkwepu na Indira Gandhi (Makunganya) jijini Dar es Salaam.

Hatua hiyo ya NHC ilitokana na mgogoro wa muda mrefu, wakimtuhumu Mbowe kushindwa kulipa deni la zaidi ya Sh. 1.3 bilioni, ikiwa jumla ya fedha za kodi ya kupangishwa kwenye jengo hilo.

Kutokana na mvutano huo, Mbowe alifungua kesi katika Mahakama Kuu, Kitengo cha Ardhi, kupinga hatua ya NHC kumuondoa katika jengo hilo, pamoja na kuchukua mali zake huku wakitangaza kuzipiga mnada baada ya siku 14 tangu kuzichukua.

Jana, Jaji Siyovelwa Mwangasi alitoa zuio na kuiamuru NHC kutouza wala kupiga mnada mali hizo za Mbowe mpaka mahakama hiyo itakapotolea uamuzi katika kesi ya msingi.

Katika kesi hiyo namba 722 ya mwaka 2016, Mbowe anawakilishwa na Mawakili  Peter Kibatala na Omary Msemo.

Jaji Mwangasi amesema kuwa, anakubaliana na maombi ya mlalamikaji na kutaka mali hizo zisiuzwe hadi hapo mahakama itakapofanyia uamuzi kesi ya msingi.

Hatua hiyo inakuja baada ya upande wa NHC kupitia mawakili wake Aloyce Sekule na Miriam Mungula kushindwa kuwasilisha hoja za msingi kueleza, ni kwanini zuio hilo lisitolewe hadi hapo kesi ya msingi itakapoanza kusikilizwa.

Awali, mawakili wa NHC, walidai kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza maombi ya Mbowe kwa kuwa hakuna kesi ya msingi ambayo imefunguliwa, hivyo maombi hayo yatupiliwe mbali.

Wakili Kibatala alijibu hoja hiyo kwa kusema, hatua ya kuwasilisha maombi hayo inalenga kubaini kama kweli Mbowe anadaiwa kodi ama la.

Kibatala alidai kuwa mahakama hiyo ina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo, hivyo inaweza ikatoa uamuzi wowote, na ndiyo maana wamewasilisha maombi hayo ili itolewe amri ya muda ya kuzuia mchakato huo.

Miongoni mwa hoja za Mbowe alizoziwalisha mahakamani hapo, ni pamoja na hoja kuwa, yeye (Mbowe) na shirika hilo walikubaliana kwamba atalikarabati na kulipanua jengo hilo kwa asilimia 100. Makubaliano ambayo yaliingiwa mwaka 1997.

Amedai kuwa katika makubaliano hayo yeye na NHC walikubaliana watamiliki jengo hilo kwa pamoja kwa muda wa miaka 99, huku Mbowe katika mgawanyo wa mapato akitakiwa kupata asilimia 75 na NHC ikitakiwa kupata asilimia 25.

Pia alieleza kuwa katika makubaliano hayo, licha ya mwenendo wa kibiashara kutokuwa mzuri, muda wote alikuwa akilipa asilimia hiyo 25, kwa mujibu wa makubaliano yao.

Hivyo kutokana na hatua ya NHC kuvunja mkataba huo kwa kumtoa kwenye jengo na kuchukua mali zake, anaiomba mahakama iliamuru shirika hilo limlipe fidia.

Mbowe aliondolewa kwenye jengo husika mnamo Septemba mosi kwa madai ya kushindwa kulipa deni la zaidi ya Sh. bilioni 1.3.

Mawakala wa NHC walifika katika jengo hilo saa 12:30 asubuhi na wafanyakazi zaidi ya 50 na kwenda moja kwa moja katika kampuni ya Free media pamoja na ukumbi wa Bilcanas na kuchukua vifaa mbalimbali ikiwemo, meza, viti na kompyuta.

Siku chache baada ya kuondolewa kwa Mbowe katika jengo hilo, Rais John Magufuli alilisifu shirika hilo kwa hatua hiyo na kulitaka lichukue hatua kama hizo kwa wadaiwa wengine zikiwemo taasisi za umma

 

Friday, September 9, 2016

Polisi Wamhoji Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Boniface Jacob


SeeBait


Maofisa wa Polisi wamemhoji Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Boniface Jacob kabla ya hajakutana na waandishi wa habari kwa madai kuwa wamepata taarifa mkutano wake huo ulilenga kumkashifu Rais John Magufuli.

Maofisa hao waliovalia kiraia walionana na Jacob ofisini kwake na walimruhusu kuendelea na mkutano huo baada ya meya huyo kuwahakikishia kwamba hana nia hiyo bali alitaka kutoa ufafanuzi wa baadhi ya masuala baada ya ujio wa Rais, Kinondoni Jumanne iliyopita.

“Kwa mara ya kwanza meya anahojiwa, lakini niliwaambia wana usalama lengo langu ni nini na sipo kwa ajili ya kumkashifu Rais, ila nafahamu vita iliyopo kati yetu na baadhi ya viongozi,” alisema Jacob.

Pamoja na ufafanuzi huo, Jacob aliwataka baadhi yao (askari) kushiriki kwenye mkutano huo wa wanahabari kufuatilia alichotaka kuwaeleza wanahabari na polisi mmoja alibaki kusikiliza bila kutambulishwa.

Kamanda wa Polisi wa Kinondoni, Suzan Kaganda alisema hakukuwa na tatizo lolote polisi kuwapo eneo  hilo, kwani wanafanya shughuli zao za ulinzi na usalama wa raia na hasa ikizingatiwa kuwa kuna Ofisi ya Mkuu wa Wilaya.

Katika mkutano huo, meya Jacob alitoa ufafanuzi wa yaliyojiri Jumanne iliyopita wakati Rais Magufuli alipofanya ziara katika manispaa hiyo na kubatilisha umiliki wa eneo la Magomeni Kota lililokuwa mali ya halmashauri kuwa ya Serikali Kuu.

Meya Jacob aliwaambia wanahabari kuwa uamuzi wa Serikali kuchukua eneo hilo umeisababishia halmashauri yake hasara ya zaidi Sh4.5 bilioni kutokana na gharama walizoingia. 

Katika eneo hilo, nyumba 644 zilivunjwa mwaka 2011 kwa miadi ya kwamba zikijengwa upya, wananchi waliokuwa wakiishi hapo wakiwa wapangaji wangerejeshwa, lakini mradi huo ulichelewa kuanza.

Akiwa ameambatana na baadhi ya madiwani, Jacob alisema hasara hiyo imetokana na halmashauri kutumia Sh2 bilioni kumlipa mkandarasi kwa ajili ya michoro ya eneo litakavyokuwa. 

Alisema pia manispaa hiyo imetoa Sh1 bilioni kwa mkandarasi Gulf kwa ajili ya kuchora ramani ya ofisi mpya za halmashauri na kusimamia ujenzi wa mradi huo na kutumia Sh700 milioni kuwalipia kodi wapangaji hao baada ya kuwahamisha.

“Faida tuliyoipata ni kwamba wananchi tuliopanga kuwahudumia tayari Rais amewahudumia. Hatupingi maamuzi ya Serikali, lakini wananchi watambue kwamba manispaa haina chochote itakachokipata, bali kila kitu kitakuwa kinafanywa na Serikali Kuu,” alisema Jacob.

Meya alisisitiza kuwa madiwani wa Ukawa hawapingi uamuzi huo ila baadhi ya viongozi wanaomzunguka Rais hawamwambii ukweli wa mambo kuhusu mradi wa Magomeni Kota na kwamba baadhi ya watumishi wa Serikali ndiyo waliosababisha kufikia hatua hiyo.

“Siku ile ningepata nafasi hata dakika tatu, ningemweleza Rais Magufuli ukweli wa mambo wa mradi huu. Lakini kuna baadhi ya viongozi waliomzunguka waliamua kuninyima nafasi hiyo. "

Hata hivyo, Jacob alimwomba Rais Magufuli kukutana naye ili amweleze kwa undani jambo linalomuumiza kuhusiana na masuala ya ardhi yanayoikumbuka Kinondoni.

Alifafanua kwamba, Serikali iliyopita na manispaa hiyo ilishaingia mkataba na kampuni ya Blue Marine ya Romania kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa Magomeni Kota ambao ulifikia katika hatua nzuri lakini baadhi ya watumishi wa Serikali waliamua kuweka ‘kauzibe’ na kuipa sifa mbaya Kinondoni.

“Tulikuwa tunasubiri utiaji wa saini kutoka Serikali Kuu, lakini baada ya kuona Kinondoni inaongozwa na Ukawa wameamua kuleta ‘figisufigisu’ za kuukwamisha,” alisema Jacob.

Katika ziara hiyo, Rais Magufuli alielezea kusikitishwa kwake na namna tatizo la wakazi hao lilivyoshughulikiwa na kuwaahidi kuwa Serikali yake itahakikisha hawasumbuliwi.

 Friday, September 9, 2016

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 9


SeeBait

Reviewed by RICH VOICE on Septemba 09, 2016 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...