Wednesday, September 14, 2016


Rais Dkt. Magufuli Amuapisha Balozi Dk. Dau Pamoja Na Makatibu Tawala Wa Mikoa Mitatu Ikulu Jijini Dar Es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 14 Septemba, 2016 amemuapisha Dkt. Ramadhani Kitwana Dau kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malaysia.

Kabla ya kuteuliwa kuwa Balozi, Dkt. Ramadhan Kitwana Dau alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF)

Mhe. Balozi Dkt. Ramadhani Kitwana Dau anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Malaysia Dkt. Aziz Ponary Mlima ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Wakati huo huo, Rais Dkt. John Pombe Magufuli, amewaapisha Makatibu Tawala wa Mikoa mitatu aliowateua mwishoni mwa wiki iliyopita.

Walioapishwa ni  kwanza, Bw. Eliya Mtinangi Ntandu anayekuwa Katibu Tawala wa kwanza wa Mkoa wa Songwe ulioanzishwa rasmi Mwezi Februari 2016.

Pili, Bw. Adoh Stephen Mapunda anayekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara.

Bw. Adoh Stephen Mapunda anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Benedict Richard Ole Kuyan ambaye amestaafu.

Tatu, Bw. Tixon Tuliangine Nzunda anayekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa.

Bw. Tixon Tuliangine Nzunda anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Symthies Emmanuel Pangisa ambaye amestaafu.

Baada ya kuapishwa, Mhe. Balozi Ramadhani Kitwana Dau na Makatibu Tawala wote watatu wamekula Kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi wa Umma kilichoongozwa na Kamishna wa Maadili Jaji Mstaafu Salome Kaganda na kushuhudiwa na Rais Magufuli.

Matukio yote yamefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es Salaam
14 Septemba, 2016


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Bw. Tixon Nzunda kuwa Katibu Tawala wa mkoa wa Rukwa, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Bw. Eliya Ntandu kuwa Katibu Tawala mkoa wa Songwe, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Balozi mpya wa Tanzania nchini Malaysia Dkt. Ramadhani Dau mara baada ya tukio la uapisho Ikulu jijini Dar es Salaam.

 

 

Wednesday, September 14, 2016


Majambazi Yavamia Magari ya Mnadani na Kumuua Dereva Mmoja kwa Risasi


Majambazi wapatao 10 juzi usiku walivamia magari mawili yaliyobeba wafanyabiashara waliokuwa wakitokea mnadani na kumuua kwa risasi, dereva aliyegoma kuwapa fedha na simu.

Dereva huyo, Chrispin Inyangwe (40) alipigwa risasi ya mgongoni alipojaribu kupambana nao.

Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana eneo la katikati ya vijiji vya Miula na Kalundi vilivyopo Kata ya Kipande wilayani Nkasi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando alisema wafanyabiashara hao walikuwa wakitokea mnadani na walipofika eneo hilo walikuta mawe yamepangwa barabarani kuzuia magari.

Alisema baada ya kuona mawe hayo, magari hayo yalilazimika kusimama na ndipo majambazi hao waliokuwa na silaha za moto, mapanga na marungu walipoibuka na kufyatua risasi hewani na baadaye kutaka wafanyabiashara hao wasalimishe fedha na simu zao za mkononi.

Kamanda huyo alisema baadhi ya wafanyabiashara walisalimisha fedha na simu zao, na waliokataa walishambuliwa.

Inasemekana kwamba Inyangwe ambaye alikuwa dereva wa gari aina ya Mitsubishi Canter alikaidi kutoa fedha na kutaka kupambana nao, ndipo watu hao waliokuwa na bunduki aina ya SMG walipomfyatulia risasi iliyompata mgongoni na kufariki dunia papo hapo.

Kitendo hicho kiliwafanya wafanyabiashara wengine waliokuwa wakikataa kutoa fedha, kuzisalimisha sambamba na simu zao, ndipo majambazi hao walipowaachia na kukimbia.

Watu 19 waliojeruhiwa walipelekwa Hospitali ya Mkoa mjini Sumbawanga. Kamanda Kyando alisema majeruhi 12 waliruhusiwa kurejea nyumbani na wengine saba wanaendelea na matibabu na kwamba polisi wanaeendelea na msako wa watu hao.

 

 

Wednesday, September 14, 2016


Wakurugenzi Wapya 13 Waapishwa.....Watakiwa kufuatilia maagizo ya viongozi


SeeBait
Wakurugenzi wapya 13 wa halmashauri wameapa kulinda maadili na kukabidhiwa majukumu ya kufuatilia maagizo ya Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu, kwenye maeneo yao na kutoa mrejesho wa hatua za utekelezaji wake. 
Kiapo hicho kilihudhuriwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Angela Kairuki aliyewataka kutilia mkazo ufuatiliaji wa maagizo na kupambana na tatizo la watumishi hewa ambao idadi yao imefikia 17,102 waliogundulika katika kipindi cha kuanzia Machi mpaka sasa. 

Wakurugenzi hao walioteuliwa hivi karibuni na Rais, John Magufuli waliapishwa jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene katika ukumbi wa Tamisemi mjini Dodoma.

 Akizungumza mara baada ya kiapo hicho, waziri Kairuki aliwataka wakurugenzi hao kutekeleza matamko yote yanayotolewa na viongozi wa ngazi za juu serikalini, kwa kutoa mrejesho wa utekelezaji wake. 

Kairuki aliwataka kufanya kazi kwa bidii ili wawatumikie wananchi wanaowaongoza. 

Alisema katika ziara nyingi alizozifanya, amekuta wakurugenzi hawafuatilii matamko yanayotolewa na viongozi wa ngazi za juu serikalini katika maeneo yao. 

“Hata kwa wale ambao wanayafuatilia huwa hawatoi mrejesho wa hatua zilizofikiwa katika kutekeleza matamko hayo, hivyo ninawaomba mkayatekeleze maagizo na kurudisha mrejesho kwa kiwango kinachotakiwa,” alisema Kairuki. 

Pia, aliwataka wakurugenzi hao kwenda kusimamia fedha za miradi ya maendeleo zinazotolewa na Serikali hadi senti ya mwisho, ili kuhakikisha inatekelezwa kwa asilimia 100. 

Alisema kuna baadhi ya miradi ya maendeleo, inatekelezwa kwa fedha za Serikali na wakati huo huo inatumia fedha za wafadhili. 

Waziri Kairuki aliwataka wakurugenzi hao kuhakikisha kuwa miradi yote inayotumia fedha za Serikali inasimamiwa ipasavyo. 

“Utakuta mradi mmoja unafadhiliwa na pia unatumia fedha za Serikali, kwa hiyo wafadhili wakija kukagua wanaonyeshwa jengo likiwa limekamilika na Serikali nayo ikija kukagua inaonyeshwa jengo hilohilo. Nataka mkasimamie fedha zote za Serikali kwenye mamlaka zenu,” alisema Kairuki. 

 Alisema kuna baadhi ya maeneo ambako fedha za Tasaf (mpango wa kunusuru kaya maskini), zimetumika kujengea maabara na kununulia madawati kinyume na malengo yaliyokusudiwa. 

Pia, aliwataka kuhakikisha kuwa hatua kali za kinidhamu zinachukuliwa kwa wakati kwa watumishi waliosimamishwa kazi katika kipindi cha miezi sita na si zaidi ya hapo. 

Alisema mtumishi aliyechukuliwa hatua za kinidhamu ikiwamo kufukuzwa au kusimamishwa kazi, mchakato wake wote ufanyike ndani ya miezi sita. 

Aliwataka pia wakurugenzi hao kufuata maadili ya viongozi wa umma, kwani wakikiuka watafikishwa kwenye baraza la maadili ya viongozi wa umma ambalo kwa sasa limeongezewa meno. 

Waziri Kairuki aliwataka wakurugenzi hao kusimamia suala la rasilimali watu, kwani utafiti ulionyesha kuwa asilimia 80 hadi 90 ya watumishi wa umma ni watoro.

Alisema katika baadhi ya maeneo kuna wakaguzi na waratibu wa elimu wa kata, lakini hawatembelei shule zao kuona kama walimu wanahudhuria shuleni au la. 

Kadhalika, aliwataka wakurugenzi hao kuachana na tabia ya kuwatumia viongozi wa Serikali walioko chini yao, kama vile watendaji wa kata, vijiji na wenyeviti wa vijiji kuwalimia mashamba yao.

Alisema watakaobainika kufanya vitendo hivyo, watachukuliwa hatua kali za kinidhamu. 

Waziri Simbachawene aliwataka wakurugenzi hao kwenda kuchapa kazi bila kumwonea yeyote. Aliwaambia kuwa kukusanya  mapato kiwe ni kipaumbele chao cha kwanza, kwani kipimo cha mamlaka yoyote kujitegemea ni uwezo wake wa kukusanya mapato. 

Aliwataka wakurugenzi hao kuhakikisha kuwa wanawatembelea watumishi wao wote ili kujua penye upungufu, idadi yao na hata ikiwezekana kuwajua kwa majina yao. 

Wakurugenzi walioapishwa jana ni Godwin Kunambi (Dodoma) Elias Ntiruhungwa (Tarime), Mwantumu Dau (Bukoba) na Frank Bahati (Ukerewe) Wengine ni Hudson Kamonga (Mbulu), Mwailwa Pangani (Nsimbo), Godfrey Sanga (Mkalama), Yusufu Semuguruka (Ulanga), Bakari Mohamed (Nachingwea), Juma Mnweke (Kibondo), Butamo Ndalahwa (Moshi), Waziri Mourice (Karatu) na Fatma Latu (Bagamoyo). 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mhe. George Simbachawene.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Angella Kairuki akiongea Wakurugenzi wapya mara baada ya kuapishwa jana mjini Dodoma. Kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mhe. George Simbachawene. Kushoto kwa Simbachawene ni  Mkurugenzi mteule wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilimanjaro Bi. Butamo Nuru Ndalahwa

 

Wednesday, September 14, 2016


Wanafunzi Wacharaza Viboko Walimu Wao ........Mmoja Ang'olewa Meno Matano, Mwingine Ngeu Kichwani


Waziri wa Elimu, Prof Joyce Ndalichako
Wawanafunzi wa Kidato cha Sita Shule ya Sekondari Usevya wilayani Mlele Mkoa wa Katavi, wanadaiwa kuwashambulia kwa kuwacharaza viboko walimu wao wawili miongoni mwao akiwemo Makamu Mkuu wa Shule hiyo, Makonda Ng’oka “Membele'‘ (34) ambaye ameng’olewa meno matano kwa kipigo hicho.

Walimu hao wawili wamedai kuwa hawako tayari kuendelea kufundisha katika shule hiyo huku wakisisitiza kuwa ni fedheha kwao kucharazwa viboko na wanafunzi wao wenyewe ambapo Mwalimu Gabriel Kambona aliachwa na ngeu kichwani.

Mei mwaka huu, Ng’oka “Membele” alifikishwa katika Mahakama ya Mkoa wa Katavi kwa tuhuma za kumlawiti mwanafunzi wake akidaiwa kutenda kosa hilo kati ya Novemba 2015 na Aprili mwaka huu.

Ilisemekana kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa Makamu Mkuu huyo wa shule hiyo kulifuatia wanafunzi wa kiume wanaosoma Kidato cha Tano sasa wako Kidato cha Sita katika shule hiyo kumkataa na kutishia kuandamana kupinga vitendo vyake vya kuwalawiti wanafunzi wake.

Wanafunzi hao walidai kuwa mwalimu huyo amekuwa akiwalawiti baadhi yao ikiwa ni adhabu mbadala wanapobainika kufanya makosa shuleni hapo.

Hata hivyo, baada ya kutopatikana ushahidi wa kumtia hatiani Ng’oka, Julai 27, mwaka huu Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Mpanda ilimwachia huru.

Mwalimu Ng’oka aliripoti kwenye kituo chake cha kazi shuleni Usevya Agosti Mosi mwaka huu ambako kurejea kwake shuleni hapo kunadaiwa kuamsha hasira kwa baadhi ya wanafunzi wa Kidato cha Sita wakidai hawapo tayari kumwona mwalimu huyo na familia yake shuleni hapo.

Akizungumza na wanahabari jana mjini hapa, Ng’oka alidai kuwa hayuko tayari kuendelea kufundisha kwenye shule hiyo akihofia usalama wake na kutokana na kipigo alichokipata cha kushambuliwa na baadhi ya wanafunzi wake wa kidato cha tano na cha sita wakati akiwa nyumbani kwake na familia yake.

 Akisimulia mkasa huo, alisema Agosti 12, mwaka huu usiku alikuwa nyumbani kwake shuleni hapo pamoja na familia yake pamoja na mwalimu mwenzake, Gabriel Kambona aliyekuwa amemtembelea.

“Ghafla, saa mbili usiku nikiwa maliwatoni nikioga lilitokea kundi la wanafunzi wa kidato cha tano na sita wakiwa na silaha za jadi kama vile fimbo, marungu, mawe na matofali na kuanza kuishambulia familia yangu pamoja na mwalimu Kambona,” alieleza na kuongeza kuwa alilazimika ‘kuchomoka’ bafuni baada ya kusikia mayowe yaliyokuwa yakipigwa na familia yake wakiomba msaada. Alipofika sebuleni alishuhudia wanafunzi hao wakiishambulia familia yake kwa kuwacharaza viboko.

“Ndipo walinigeukia na kuanza kunishambulia kwa kunipiga kwa marungu na fimbo hadi nikapoteza fahamu nilizinduka nikiwa nimelazwa kwenye Kituo cha Afya Usevya na kubaini kuwa nimepoteza meno yangu matano huku nikiwa nimejeruhiwa vibaya kichwani. Baadaye nilihamishiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda ambako nililazwa wiki moja na nusu kwa matibabu na sasa nimepewa rufaa niende Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar kwa matibabu zaidi,” alieleza.

Alidai kuwa uhasama baina yake na wanafunzi hao umedumu kwa muda mrefu, lakini anashangaa uongozi wa Halmashauri ya Mpimbwe na Wilaya ya Mlele umeshindwa kumpangia kituo kingine cha kazi na kuchukua hatua yoyote kwa wanafunzi hao licha ya kupeleka majina yao kwa kuwa anawafahamu wote waliohusika.

Mwalimu Kambona alidai kuwa hayuko tayari kuendelea kufundisha kwenye shule hiyo kwamba kitendo cha kupigwa na wanafunzi wake kimemfedhehesha.

Kwa mujibu wa mwalimu huyo, walimu wa shule hiyo waliketi baada ya kutokea kwa tukio hilo, na walifikia maamuzi kuwa wanafunzi wote waliobainika kushiriki kuwashambulia walimu wao wasimamishwe shule akidai kuwa uongozi wa Halmashauri ya Mpimbwe na Wilaya ya Mlele ulipinga.

“Nimeandika barua ya kuomba uhamisho kwani nia aibu kwangu kuendelea kufundisha wanafunzi ambao wamenishambulia na kunitoa ngeo kichwani ….. siku hiyo ya tukio niliibiwa simu mbili za kiganjani lakini jana nimefanikiwa kuikamata simu moja kwa mwanafunzi wa kidato cha tano anayeitwa , Alex Maiko Makona na tayari amemfikisha katika Kituo cha Polisi cha Usevya,” alidai.

Mwenyekiti wa Chama cha Walimu (CWT) Mkoa wa Katavi, Gregori Mshota alisema tayari chama chake kimeanza kuwasiliana na uongozi wa Halmashauri ya Mpimbwe na uongozi wa Wilaya ya Mlele ili kuhakikisha mwalimu huyo anakuwa salama.

Ofisa Elimu wa Mkoa wa Katavi, Ernest Hinju alidai kuwa suala hilo lipo ofisini kwake na wameanza kulitafutia ufumbuzi. “Jambo hili linahitaji ushirikishwaji wa vyombo mbalimbali ikiwemo Bodi ya Shule ya Sekondari ya Usevya,” alieleza.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipokuwa katika ziara mkoani Katavi mwezi uliopita, mke wa mwalimu Ng’oka alitinga kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini Maji Moto akiwa na bango lenye malalamiko ya kutishiwa usalama wa maisha wa familia yake, na Waziri Mkuu alimwagiza Kamanda wa Polisi wa Mkoa kushughulikia malalamiko hayo.

 

 

 

 

Wednesday, September 14, 2016


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Apokea Zaidi Ya Sh. Bil. 1.4 Kwa Ajili Ya Maafa Ya Tetemeko La Kagera


agera imefungua akaunti maalumu katika benki ya CRDB kwa ajili ya kupokea michango kutoka kwa watu mbalimbali. Namba za akaunti hiyo ya Kamati ya Maafa ya Kagera ni CRDB 0152225617300.

Pia Waziri Mkuu aliwapongeza na kuwashukuru waheshimiwa Wabunge kwa kuamua kutoa posho zao za kikao cha jana kwa ajili ya kuchangia wahanga wa tetemeko hilo na kuwaomba wananchi wengine kujitokeza na kutoa michango yao.

Wakati huo huo viongozi wa makampuni ya mafuta ya GBP, Oil Com na Moil wameahidi kujenga shule mbili za Nyakato na Ihungo ambazo sehemu kubwa ya miundombinu yake imeharibika vibaya. Shule hizo zitajengwa katika kipindi cha siku 30.

Hafla hiyo iliyoongozwa na Waziri Mkuu ilihudhuriwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Suzan Kolimba na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi, Dk. Aziz Mlima.

 

 

 

Wednesday, September 14, 2016


Namba ya akaunti ya kuwachangia walioathiriwa na tetemeko la ardhi Kagera


SeeBait

 

Wednesday, September 14, 2016


Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya Septemba 14






katika habari za kimataifaaa

Habari | 14.09.2016 | 10:10


Mkuu wa Halmashauri ya Umoja wa Ulaya, Jean-Claude Juncker, amehimiza mshikamano katika Umoja wa Ulaya baada ya kujiondoa kwa Uingereza, akisema ingawa Ulaya haikabiliwi na kitisho cha kugawanyika, inapaswa kufanya kazi pamoja. Katika hotuba yake mbele ya Bunge la Ulaya, ambayo imezigusia sera kadhaa ya kisiasa na za kiuchumi, 
Juncker amezitaka nchi za Ulaya kushirikiana kupambana na wimbi la siasa kali za kizalendo zinazoshika kasi.
 Hotuba yake imetolewa siku mbili kabla ya mkutano wa kilele wa nchi za Umoja wa Ulaya ambao utafanyiuka katika mji mkuu wa Slovakia, Bratislava, wa kwanza  bila wawakilishi wa Uingereza.

 Mkutano huo unatarajiwa kuchora ramani ya mwelekeo wa Umoja wa Ulaya, baada ya kujiondoa kwa Uingereza. Jean-Claude Juncker ameitumia hotuba hiyo kuitaka Uingereza kuanzisha rasmi mchakato wa kujiondoa katika Umoja wa Ulaya, haraka iwezekanavyo. 


Mpango wa kusitisha mapigano nchini Syria unaoenekana kuendelea kuheshimiwa, masaa zaidi ya 36 baada ya kuanza kutekelezwa, limesema shirika la kuchunguza haki za binadamu nchini Syria lenye makao nchini Uingereza, na kuongeza hata hivyo kuwa watu wenye mahitaji makubwa bado hawajafikiwa na msaada.
 Mpango huo uliofikiwa katika makubaliano baina ya Marekani na Urusi, unavihusu vikosi vya serikali na vya waasi, lakini unalitenga kundi linalojiita Dola la Kiislamu, IS, na mengine yenye mafungamano na mtandao wa kigaidi wa al-Qaida. 
Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, watu wapatao 275,000, mashariki mwa mji wa Aleppo wamekuwa katika mzingiro tangu mwezi Julai bila uwezekano wa kufikishiwa msaada.
 Afisa wa Umoja wa huo amesema bado wanasubiri ruhusa ya serikali ili kuwapelekea msaada wa kibinadamu watu hao.
 Serikali mjini Damascus imeeleza bayana kuwa haitaruhu kupelekwa kwa msaada kutoka Uturuki, ambayo ni hasimu wake na mshirika mkubwa wa waasi.


Ripoti ya bunge la Uingereza iliyochapishwa leo imesema uingiliaji kati nchini Libya ulioidhinishwa na aliyekuwa waziri mkuu wa nchi hiyo, David Cameron, ulitokana na taarifa potofu za kijasusi, na uliharakisha kusambaratika kwa taifa hilo lililo kaskazini mwa Afrika, kisiasa na kiuchumi. 

Mwanzoni mwa mwaka 2011, Uingereza na Ufaransa ziliongoza kampeni ya kimataifa kumuondoa madarakani aliyekuwa rais wa Libya, Muammar Gaddafi, wakitumia ndege za kivita kuyarudisha nyuma majeshi yake, na kuwaruhusu waasi kuuangusha utawala wake wa miaka zaidi ya 40.

 Mwenyekiti wa kamati ya bunge la Uingereza iliyoiandika ripoti hiyo, Crispin Blant, amesema David Cameron alikuwa na mchango katika maamuzi ya kuingilia kati nchini Libya, na anapaswa kubeba lawama za mchango wa Uingereza katika mzozo wa Libya.


Rais wa zamani wa Israel, Shimon Peres, ambaye alipelekwa hospitali jana akiwa na ugonjwa wa kiharusi, leo hii amelezewa kuwa katika hali mahtuti, lakini iliyotulia. 
Rafi Walden, daktari wa kiongozi huyo amesema Peres mwenye umri wa miaka 93 hakabiliwi tena na kitisho kwa maisha yake, akiongeza kuwa alikuwa akiweza kufahamu yanayozungumzwa kumhusu. Aidha, daktari huyo amesema Shimon Peres ambaye pia ni mshindi wa tuzo ya Nobel ya Amani kwa wakati huu amepewa dawa za kumtuliza ili ubongo wake ulioathiriwa vibaya na kiharusi uweze kupata nafuu haraka. 
Peres alikimbizwa hospitalini mjini Tel Aviv  jana baada ya kupata maumivu makali ya kichwa kufuatia hotuba ya saa nzima aliyokuwa ameitoa. 
 Kiongozi huyo mkongwe vile vile aliwahi kuwa waziri mkuu wa Israel kati ya mwaka 1984 na 1986.


Mkutano wa kilele wa nchi za Jumuiya ya Ushirikiano wa Nchi za Pembe ya Afrika, IGAD, ulimalizika jana katika mji mkuu wa Somalia - Mogadishu, kwa kutoa maazimio ya kutaka kuimarishwa kwa vikosi vya Umoja wa Afrika na vya serikali ya Somalia, ili kuweza kukabiliano na kitisho cha ugaidi, na kuyakomboa maeneo yanayosalia mikononi mwa wanamgambo wa al-Shabaab. 
Huo ulikuwa mkutano wa kwanza wa aina hiyo kufanyika mjini Mogadishu tangu mwaka 1991, wakati taifa hilo lilipotumbukia katika mzozo wa kivita.
 Viongozi katika mkutano huo pia walizungumzia uchaguzi mkuu ujao nchini Somalia, mgogoro ulioibuka upya nchini Sudan Kusini, na kuhimiza wakimbizi wa Somalia kurejea nyumbani kwa hiari yao.
 Nchi wanachama wa jumuiya ya IGAD ni pamoja na Kenya, Ethiopia, Uganda, Djibouti, Sudan na Somalia.

katika habari za kimichezo na burudani

KADI NYEKUNDU – GIROUD AMLAUMU VERRATI KWA WOTE KUTUPWA NJE!


RC-GIROUD-VERATTISTRAIKA wa Arsenal Olivier Giroud amemlaumu Kiungo wa Paris Saint-Germain Marco Verratti baada ya wote kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu baada ya kuvaana kwenye Mechi ya Kundi A la UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI Jana Usiku huko Parc des Princes, Paris iliyomalizika 1-1.
Wawili hao walilambwa Kadi za Njano za Pili katika Dakika za Majeruhi na Refa Viktor Kassai wa Hungary na kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu.
Tukio hilo lilitokea baada ya Giroud kumwangusha Verratti na kisha Marquinhos wa PSG kumsukumiza mwenzake Verrati kwa Giroud na kusababisha Refa Kassai kuwapa Kadi wote Wawili.
Baadae Giroud akalamika: “Nikiwa kwenye Kadi ya Njano, sikutaka kuleta rabsha. Nilimzuia Verratti nay eye akajirusha chini, sikuelewa hilo. Marquinhos alinisukuma toka nyuma na sijui kwanini Verratti ajiangushe mara ya pili. Hilo lilikuza tukio. Inasikitisha na hasa sijui kama Refa aliona vizuri tukio lenyewe!”
Kwenye Mechi hiyo, Edinson Cavani aliipa PSG Bao baada ya Sekunde 42 na Alexis Sanchez kuisawazishia Arsenal kwenye Dakika ya 78.
UEFA CHAMPIONZ LIGI
Matokeo:
Jumanne 13 Septemba 2016
KUNDI A
Basel 1 Ludo Razgrad 1                 
Paris St Germain 1 Arsenal 1                  
KUNDI B
Benfica 1 Besiktas 1           
Dynamo Kiev 1 Napoli 2               
KUNDI C
Barcelona 7 Celtic 0            
Man City v Borussia Monchengladbach [ILIAHIRISHWA, KUCHEZWA LEO]            
KUNDI D
Bayern Munich 5 FC Rostov 0                   
PSV Eindhoven 0 Atletico Madrid 1


UEFA CHAMPIONZ LIGI: LEO LEICESTER DIMBANI KWA MARA YA KWANZA, SPURS NA MONACO, MTANANGE JUVE-SEVILLA, KIPORO CHA CITY LEO PIA!


UEFA CHAMPIONZ LIGI
Jumatano 14 Septemba 2016
*Mechi zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku, Bongo Taimu
KUNDI E
Bayer Leverkusen v CSKA           
Tottenham v Monaco                  
KUNDI F
Legia Warsaw v Borussia Dortmund                
Real Madrid v Sporting Lisbon               
KUNDI G
Club Brugge v Leicester City                 
FC Porto v FC Copenhagen          
KUNDI H
Juventus v Sevilla             
Lyon v Dinamo Zagreb 
KUNDI C
Man City v Borussia Monchengladbach [ILIAHIRISHWA JANA]                           
++++++++++++++++++++++++++++++           
UCL-2014-15-LOGO-1Mechi za Kwanza za Makundi E hadi H ya UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, pamoja na ile iliyoahirishwa Jana kutokana na Mvua ya Kundi C kati ya Man City na Borussia Monchengladbach zitachezwa Leo Usiku,
Timu mbili za England, Mabingwa Leicester City na Tottenham, Leo wapo dimbani kwa Tottenham kucheza Uwanja wa Wembley badala ya ule wa kwao White Hart Lane, Jijini London kwa kuwavaa AS Monaco ya France kwenye Mechi ya Kundi E na Leicester City, wakicheza UCL kwa mara ya kwanza kabisa katika Historia yao, wako Ugenini huko Belgium kuivaa Club Brugge kwenye Mechi ya Kundi G.
Mechi kali hii Lo ni ya Kundi H huko Jijini Turin Nchini Italy kati ya Juventus na Mabingwa wa UEFA EUROPA LIGI Sevilla ya Spain.
Nao Mabingwa Watetezi Real Madrid, ambao wapo Kundi F, wapo kwao Santiago Bernabeu, kucheza na Sporting Lisbon ya Ureno ambayo ndiyo Timu Staa wa Real Cristiano Ronaldo alikoanzia Soka la Kulipwa.
Mechi nyingine ya Kundi F ni kati ya Legia Warsaw na Borussia Dortmund.
UEFA CHAMPIONZ LIGI
Matokeo:
Jumanne 13 Septemba 2016
KUNDI A
Basel 1 Ludo Razgrad 1                 
Paris St Germain 1 Arsenal 1                  
KUNDI B
Benfica 1 Besiktas 1           
Dynamo Kiev 1 Napoli 2               
KUNDI C
Barcelona 7 Celtic 0            
Man City v Borussia Monchengladbach [ILIAHIRISHWA, KUCHEZWA LEO]            
KUNDI D
Bayern Munich 5 FC Rostov 0                   
PSV Eindhoven 0 Atletico Madrid 1
Ratiba:
Jumanne 27 Septemba 2016
KUNDI E
CSKA v Tottenham           
Monaco v Bayer Leverkusen                  
KUNDI F
Borussia Dortmund v Real Madrid          
Sporting v Legia Warsaw            
KUNDI G
FC Copenhagen v Club Brugge              
Leicester City v FC Porto             
KUNDI H
Dinamo Zagreb v Juventus          
Sevilla v Lyon                   
Jumatano 28 Septemba 2016
KUNDI A
Arsenal v Basel                
Ludo Razgrad v Paris St Germaine                   
KUNDI B
Besiktas v Dynamo Kiev             
Napoli v Benfica               
KUNDI C
Borussia Monchengladbach v Barcelona           
Celtic v Man City              
KUNDI D
Atletico Madrid v Bayern Munich            
FC Rostov v PSV Eindhoven        
TAREHE MUHIMU:
MECHI ZA MAKUNDI:
Mechi ya Kwanza: 13 na 14 Septemba
Mechi ya Pili: 27 na 28 Septemba
Mechi ya Tatu: 18 na 19 Oktoba
Mechi ya Nne: 1 na 2 Novemba
Mechi ya Sita: 22 na 23 Novemba
Mechi ya Sita: 6 na 7 Desemba
MECHI ZA MTOANO:
11–12/04/17: Robo Fainali, Mechi ya Kwanza
18–19/04/17: Robo Fainali, Mechi ya Pili
02–03/05/17: Nusu Fainali, Mechi ya Kwanza
09–10/05/17: Nusu Fainali, Mechi ya Pili
03/06/17: Fainali (National Stadium of Wales, Cardiff)


BARCA YAPIGA 7, BAYERN 5, ARSENAL YACHOMOA, CITY YAAHIRISHWA, KUPIGWA LEO!


UEFA CHAMPIONZ LIGI
Jumanne 13 Septemba 2016
KUNDI A
Basel 1 Ludo Razgrad 1                 
Paris St Germain 1 Arsenal 1                  
KUNDI B
Benfica 1 Besiktas 1           
Dynamo Kiev 1 Napoli 2               
KUNDI C
Barcelona 7 Celtic 0            
Man City v Borussia Monchengladbach [ILIAHIRISHWA, KUCHEZWA LEO]            
KUNDI D
Bayern Munich 5 FC Rostov 0                   
PSV Eindhoven 0 Atletico Madrid 1
++++++++++++++++++++++++++++++           
UCL-2016-17-1-1Mechi za Kwanza za Makundi A hadi D za UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI zilichezwa Jana lakini ile ya Kundi C Uwanjani Etihad Jijini Manchester kati ya Manchester City na Borussia Monchengladbach ya Germany iliahirishwa kutokana na Mvua kubwa.
Huko Nou Camp, Jijini Barcelona Nchini Spain katika Mechi nyingine ya Kundi C, na Barcelona iliitwanga Celtic ya Scotland 7-0 na huko Paris, France, kwenye Mechi ya Kundi A, Paris St Germain na Arsenal zilitoka 1-1.
Huko Munich, Germany, Mechi ya Kundi D, iliisha kwa Wenyeji Bayern Munich kuwaadhibu FC Rostov 5-0.                 
Barcelona 7 Celtic 0
Lionel Messi alipiga Bao 3, Luis Suarez 2 na Neymar na Iniesta kufunga 1 kila mmoja wakati Barcelona ikiitwanga Celtic 7-0 kwenye Mechi ya Kundi C huko Nou Camp.  
VIKOSI:
Barcelona: Ter Stegen, Pique, Umtiti, Alba, Gomes, Rakitic, Busquets, Roberto, Messi, Suarez, Neymar
Akiba: Cillessen, Arda, Iniesta, Rafinha, Mascherano, Alcacer, Digne
Celtic: De Vries, Gamboa, Lustig, Sviatchenko, Toure, Tierney, Roberts, Brown, Bitton, Sinclair, Dembele
Akiba: Gordon, Izaguirre, Armstrong, Rogic, O’Connell, McGregor, Forrest
REFA: Ovidiu Hategan (Romania)
Paris St Germain 1 Arsenal 1
Huko Parc des Princes, Paris, Nchini France, Edinson Cavani aliipa Bao PSG baada ya Sekunde 42 tu toka Gemu ianze lakini Alexi Sanchez alisawazisha na kuipa Arsenal Sare ya 1-1 katika Mechi ya Kundi A.
Mechi hii iliisha kwa kila Timu kubaki Mtu baada ya Olivier Giroud na Verratti kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu baada ya wote kupewa Kadi za Njano za Pili baada ya kuvaana Dakika za mwishoni.
VIKOSI:
PSG: Areola; Aurier, Marquinhos, Thiago Silva, Maxwell; Verratti, Krychowiak, Rabiot; Di Maria, Cavani, Matuidi
Akiba: Trapp, Kimpembe, Moura, Motta, Pastore, Meunier, Jesé
Arsenal: Ospina; Bellerin, Mustafi, Koscileny, Monreal; Cazrola, Coquelin; Iwobi, Ozil, Ozil-Chamberlain; Sanchez
Akiba: Cech, Holdig, Gibbs, Xhaka, Elneny, Lucas, Giroud
REFA: Viktor Kassai (Hungary)
Bayern Munich 5 FC Rostov 0
Huko Munich, Germany, Mechi ya Kundi D, iliisha kwa Wenyeji Bayern Munich kuwaadhibu FC Rostov 5-0.                 
Bao za Bayern zilipachikwa na Robert Lewandowski, Penati, Kimmich, Bao 2, Tomas Muller na Bernat.
UEFA CHAMPIONZ LIGI
*Mechi zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku, Bongo Taimu
Jumatano 14 Septemba 2016
KUNDI E
Bayer Leverkusen v CSKA           
Tottenham v Monaco                  
KUNDI F
Legia Warsaw v Borussia Dortmund                
Real Madrid v Sporting Lisbon               
KUNDI G
Club Brugge v Leicester City                 
FC Porto v FC Copenhagen          
KUNDI H
Juventus v Sevilla             
Lyon v Dinamo Zagreb                
Jumanne 27 Septemba 2016
KUNDI E
CSKA v Tottenham           
Monaco v Bayer Leverkusen                  
KUNDI F
Borussia Dortmund v Real Madrid          
Sporting v Legia Warsaw            
KUNDI G
FC Copenhagen v Club Brugge              
Leicester City v FC Porto             
KUNDI H
Dinamo Zagreb v Juventus          
Sevilla v Lyon                   
Jumatano 28 Septemba 2016
KUNDI A
Arsenal v Basel                
Ludo Razgrad v Paris St Germaine                   
KUNDI B
Besiktas v Dynamo Kiev             
Napoli v Benfica               
KUNDI C
Borussia Monchengladbach v Barcelona           
Celtic v Man City              
KUNDI D
Atletico Madrid v Bayern Munich            
FC Rostov v PSV Eindhoven        
TAREHE MUHIMU:
MECHI ZA MAKUNDI:
Mechi ya Kwanza: 13 na 14 Septemba
Mechi ya Pili: 27 na 28 Septemba
Mechi ya Tatu: 18 na 19 Oktoba
Mechi ya Nne: 1 na 2 Novemba
Mechi ya Sita: 22 na 23 Novemba
Mechi ya Sita: 6 na 7 Desemba
MECHI ZA MTOANO:
11–12/04/17: Robo Fainali, Mechi ya Kwanza
18–19/04/17: Robo Fainali, Mechi ya Pili
02–03/05/17: Nusu Fainali, Mechi ya Kwanza
09–10/05/17: Nusu Fainali, Mechi ya Pili
03/06/17: Fainali (National Stadium of Wales, Cardiff)


EUROPA LIGI: ALHAMISI MAN UNITED KUANZA UGENINI NA FEYERNOOD, SAMATTA NA GENK YAKE UGENINI NA RAPID!


EUROPA-LIGI-2016-17MANCHESTER UNITED wanaanza kampeni yao ya Mechi za Makundi ya UEFA EUROPA LIGI Alhamisi Usiku Ugenini huko Uwanjani De Kuip, Stadion Feijenoord Jijini Rotterdam Nchini Netherlands kupambana na Feyenoord kwenye Mechi ya Kundi A.
Mechi nyingine ya Kundi A ni kati ya Zorya Luhansk ya Ukraine wakicheza na Fenerbahçe ya Uturuki.
Timu nyingine ya England ambayo ipo kwenye Mashindano haya ni Southampton ambao wapo Kundi K na wapo Nyumbani kucheza na Sparta Praha ya Czech Republic.
TATHMINI – Feyenoord v Man United
Man United ndio kwanza wanatoka kufungwa na Man City 2-1 kwenye Mechi ya EPL, Ligi Kuu England, na Meneja wao Jose Mourinho amedokeza ataibadili Timu.
Wachezaji ambao wanatarajiwa kuanza Mechi hii ni Chipukizi Marcus Rashford na Ander Herrera ambao kwenye Mechi na City waliingizwa Kipindi cha Pili na kuleta uhai mkubwa.
Man United imeshacheza na Feyenoord mara 2, kwenye Kundi lao la UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu wa 1997/98, na Man United kushinda Mechi zote mbili ikiwemo 3-1 huko Uwanjani De Kuip ambako Andy Cole alipiga Hetitriki.
++++++++++++++++++++++++++++++++++++
MAN UNITED – Mechi zao za Kundi A:
**Saa za Bongo
MD 1 – Alhamisi Sep 15 2000 – Feyenoord v Man United
MD 2 – Alhamisi Sep 29 22:05 –  Man United v Zorya Luhansk
MD 3 – Alhamisi Okt 20 22:05 – Man United v Fenerbahce SK
MD 4 – Alhamisi Okt 27 2000 –  Fenerbahce SK v Man United
MD 5 – Alhamisi Nov 24 2305 – Man United v Feyenoord
MD 6 – Alhamisi Des 8 2100 –  Zorya Luhansk v Man United
++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Hivi sasa Feyernoord ipo chini ya Kocha Giovanni van Bronckhorst ambae ni Mchezaji wa zamani ewa Arsenal na baadae kuhamia Barecelona na kisha kurudi kwao kuichezea Feyernoord.
Kikosi cha Feyernoord kina Wachezaji kadhaa waliowahi kuzichezea Klabu za Ligi Kuu England na hao ni Dirk Kuyt, aliekuwa Liverpool, Kipa Brad Jones, ambae nae alikuwa Liverpool na Eljero Elia aliewahi kuichezea Southampton kwa Mkopo Mwaka 2015.
Nayo Timu ya Straika wa Tanzania Mbwana Samatta, Genk ya Belgium itaanza Ugenini na Rapid Wien ya Austria katika Kundi F ambapo pia wapo Sassuolo ya Italy, watakaokuwa Nyumbani, kucheza na Athletic Bilbao ya Spain.
UEFA EUROPA LIGI
Mechi za Ufunguzi
Alhamisi Septemba 15
KUNDI A: Feyenoord v Manchester United, Zorya Luhansk v Fenerbahçe
KUNDI B: Young Boys v Olympiacos, APOEL v Astana
KUNDI C: Mainz v St-Étienne, Anderlecht v Qäbälä
KUNDI D: AZ Alkmaar v Dundalk, Maccabi Tel-Aviv v Zenit
KUNDI E: Viktoria Plzeň v Roma, Astra Giurgiu v Austria Wien
KUNDI F: Rapid Wien v Genk, Sassuolo v Athletic Club
KUNDI G: Standard Liège v Celta Vigo, Panathinaikos v Ajax
KUNDI H: Konyaspor v Shakhtar Donetsk, Braga v Gent
KUNDI I: Salzburg v Krasnodar, Nice v Schalke
KUNDI J: QarabaÄŸ v Slovan Liberec, PAOK v Fiorentina
KUNDI K: Inter Milan v Hapoel Beer-Sheva, Southampton v Sparta Praha
KUNDI L: Osmanlıspor v Steaua Bucureşti, Villarreal v Zürich
TAREHE MUHIMU
Droo
26/08/16: Makundi
12/12/16: Raundi ya Mtoano ya Timu 32
24/02/17: Raundi ya Mtoano ya Timu 16
17/03/17: Robo Fainali
Makundi
15/09/16: Mechidei 1
29/09/16: Mechidei 2
20/10/16: Mechidei 3
03/11/16: Mechidei 4
24/11/16: Mechidei 5
08/12/16: Mechidei 6
16/02/17: Raundi ya Mtoano ya Timu 32, Mechi za Kwanza
23/02/17: Raundi ya Mtoano ya Timu 32, Marudiano
09/03/17: Raundi ya Mtoano ya Timu 16, Mechi za Kwanza
16/03/17: Raundi ya Mtoano ya Timu 16, Marudiano
13/04/17: Robo Fainali, Mechi za Kwanza
20/04/17: Robo Fainali, Marudiano
04/05/17: Nusu Fainali, Mechi za Kwanza
11/05/17: Nusu Fainali, Marudiano
24/05/17: Fainali (Friends Arena, Solna, Stockholm, Sweden)

 shukrani zasngu kwa soka in bongo na mpekuzi 


Reviewed by RICH VOICE on Septemba 14, 2016 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...