Saturday, September 17, 2016

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi ya Septemba 17

SeeBait



Friday, September 16, 2016

Kutoka Mahakamani: Zombe Aachiwa Huru, Mwenzake Ahukumiwa Kunyongwa Hadi Kufa

SeeBait

Mahakama ya Rufani imemhukumu kunyongwa hadi kufa aliyekuwa Mkuu wa upelelezi wilaya ya Kinondoni (OC-CID), Mrakibu wa Polisi (SP) Christopher Bageni, baada ya kumtia hatiani kwa kosa ka mauaji ya wafanyabiashara watatu wa madini kutoka Mahenge mkoani Morogoro.

Wakati Bageni akihukumiwa kitanzi, aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi mkoa wa Dar (RCO), Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Abdallah Zombe na maafisa wengine wawili wa Polisi, Ahmed Makelle na Rajabu Bakari wameachiwa huru, baada ya mahakama kuwaona kuwa hawana hatia.

Bageni amehukumiwa adhabu hiyo leo baada ya mahakama ya Rufani kukubaliana na rufaa ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

DPP alikata rufaa akipinga hukumu ya Mahakama Kuu kuwaachia huru katika kesi ya mauaji ya wafanyabiashara hao.

Wafanyabiashara hao, Savings Chigumbi, Ephraim Chigumbi, Mathias Lunkombe na dereva teksi wa Manzese, Juma Ndugu, waliuawa Januari 14,2006, kwa kupigwa risasi Mbezi Luis, Dar.
 
 

Saturday, September 17, 2016

Lipumba, Sakaya, Kambaya watuhumiwa kupanga njama za utekaji viongozi wa CUF

SeeBait
Mkurugenzi wa Uchumi na Fedha ambaye pia ni Kaimu Naibu Mkuu CUF, Bara Joran Bashange
Chama cha Wananchi (CUF) kinawatuhumu waliokuwa viongozi wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba, aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho na Magdalena Sakaya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Bara kufanya jaribio la kumteka Mkurugenzi wa Uchumi na Fedha ambaye pia ni Kaimu Naibu Mkuu CUF, Bara Joran Bashange.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma CUF inadai kuwa jana majira ya 2:30 asubuhi vijana wanaosadikiwa kuwa wa Prof Lipumba wamefanya jaribio la kutaka kumteka Bashange wakati akitoka nyumbani kwake eneo la Buguruni.

Na kwamba watekeji hao wakiwa na gari aina ya Noah yenye namba ya Usajili T 760 CEX  baada ya jaribio la kumteka, walifanikiwa kumuingiza katika gari hiyo ya NOAH iliyokuwa na vioo vyeusi (tinted).

Taarifa hiyo ilieleza kuwa Bashange alipambana na kuomba msaada kwa kuita watu waliojirani kwa yowee la kuita “Majambazi” ndipo wananchi wakalizingira gari hilo na kuweka mawe na magogo na kuita Polisi.

Baada ya Polisi kufika waliwakagua vijana hao na kuwakuta na pingu, silaha kadhaa na kitambulisho feki cha polisi.

Baada ya ukaguzi kufanyika vijana watatu walikamatwa na mmoja alifanikiwa kukimbia.

Taarifa hiyo ilifafanua kuwa mmoja kati ya vijana waliokamatwa ni mlinzi wa karibu wa Prof. Lipumba aitwaye HAJI “Mrangi” ambaye ni maarufu na anadaiwa kujulikana kwa ushiriki wake wa vitendo vya kihuni na kiharamia kama hivyo.

Hata hivyo, katika mahojiano ya awali mmoja wa vijana hao alitoa ushirikiano na kueleza kuwa wametumwa na Abdul Kambaya na kwamba anayeongoza oparesheni yao hiyo ni mtu aitwaye Athumani (Mganga wa Kienyeji na Mwalimu wa mafunzo ya Kareti) aishiye Ilala akisaidiwa na watu wengine wanaojulikana Abubakar Fambo, Mohamed Ibrahim na Hassan Kingwele ( Mlinzi wa Magdalena Sakaya (MB).

Vijana hao waliokamatwa wanakiri kuwa mipango yote hiyo Prof. Lipumba anaijua kama vile walivyoongoza mpango wa kuhujumu Mkutano Mkuu Maalumu wa CUF ulioahirishwa pale Blue Pearl Hotel, Ubungo Plaza.

Joran Bashange ameumizwa maeneo kadhaa ya mwili na anaendelea na matibabu na taarifa za ndani zinaonesha kuwa wahusika walielekezwa kumshambulia vibaya na kumuua ikiwa wangelifanikiwa kuondoka naye.

Vijana waliohusika na utekaji huo na gari lao wanashikiliwa na Polisi katika Kituo cha Polisi Buguruni.

Chama cha CUF kimelaani kitendo hicho na kimesema kinachukua hatua stahiki.

Pia Chama hicho kimesema kinaamini kuwa kwa sasa Prof. Lipumba na watu wake wamekusudia kuendesha hujuma za wazi na kuvuka mipaka ya ushindani wa kisiasa za ndani ya Chama na kujivika joho la ‘Uintarahamwe na Umungiki’ wa wazi dhidi ya Chama na kuhatarisha na kutishia usalama wa maisha ya viongozi wa Chama.

Saturday, September 17, 2016

Wanaowapigia simu polisi bila sababu Kuchukuliwa Hatua za Kisheria

SeeBait
JESHI la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, limeahidi kuwachukulia hatua kali wananchi wanaotumia vibaya simu za dharura, zenye namba 111 na 112.

Simon Sirro, Kamishina wa Jeshi la Polisi amesema kuwa watu wamekuwa wakipiga simu hizo na kutoa taarifa za uongo au kupiga simu na kisha kuwapa watoto wadogo waongee.

“Polisi tutawafuatilia wote kupitia mitandao yetu General Packet Radio Service (GPRS),inayoonyesha maeneo walipo na simu wanazotumia ili kuwakamata na kuwachukulia hatua kali za kisheria. Haiwezekani mtu apige simu halafu baada ya simu kopokelewa anaweka muziki,” amesema.

Kamanda Sirro amesema ni vyema wananchi wakaacha mzaha na matumizi ya namba hiyo ya Jeshi la Polisi kwani kwa kufanya hivyo inapunguza morali ya askari wa jeshi hilo kufanya kazi kwa kujituma.

“Wananchi wote watumie simu zetu kutoa taarifa zenye ukweli na zitafanyiwa kazi kwa wakati, wawasiliane na sisi pale wanapoona viashiria vya uhalifu ama tukio lolote linaloleta uvunjifu wa amani na siyo kupiga simu na kufanya mzaha,” amesema Sirro.
 
 

Saturday, September 17, 2016

UKUTA Waiponza Redio ya Lowassa....Yafungwa Kwa Miezi 3 na Faini ya Milioni 5

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kupitia Kamati yake ya Maudhui imekifungia kituo cha Redio 5 Arusha kwa kipindi cha miezi mitatu pamoja na kukitoza faini ya sh. Milioni 5 kwa kosa la kukiuka baadhi ya Kanuni za Huduma za Utangazaji (maudhui) kupitia kipindi chake cha Matukio kilichorushwa Agosti 25, 2016.

Kwa mujibu wa taarifa ya kamati hiyo, katika kipindi hicho Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Mh. Godbless Lema alitamka maneno ya kashfa yaliyolenga kumdhslilisha Rais John Magufuli na serikali kwa ujumla.

Wakati akisoma maamuzi ya kamati hiyo, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui Joseph Mapunda, aliongeza kuwa kituo hicho pia kilirusha maneno yaliyo tamkwa na Lema ambayo yalikuwa yakihamasisha wananchi kushiriki katika maandamano ya Ukuta yaliyopigwa marufuku na Jeshi la Polisi.

“Maneno ya Lema yalilenga kuhamasisha wananchi kupambana na jeshi la polisi na hivyo kusababisha uvunjifu wa amani na kuhatarisha usalama wa Taifa,” alisema.

Mapunda alisema uamuzi huo umetolewa na kamati hiyo baada ya kamati hiyo kusikiliza maelezo ya utetezi yaliyotolewa na wa Uongozi wa Redio 5 Arusha.

“Baada ya kusikiliza maelezo ya utetezi kamati imeridhia kuwa kipindi cha matukio kilikiuka baadhi ya kanuni za maudhui namba 5(a,b,c,d,f,h) 6(2) (b, c) na 18 (1) (b),” alisema.

Aliongeza kuwa ” kituo hicho kinatozwa faini ya sh. Milioni 5 ambazo zitatakiwa kulipwa ndani ya siku 30 kuanzia leo, kinafungiwa kwa miezi 3 na kuwekwa chini ya uangalizi maalumu kwa muda wa Mwaka 1 baada ya kipindi cha kufungiwa kumalizika, “

Hata hivyo, Mapunda alisema haki ya wahusika kukata rufaa dhidi ya uamuzi huo iko wazi ndani ya siku 30 kuanzia leo.

Kwa upande wa kituo cha redio cha Magic Fm ambacho nacho pia kwa mujibu wa kamati hiyo kinadaiwa kukiuka kanuni za maudhui kupitia kipindi chake cha Morning Magic kipengele cha Paka Rangi ambapo kilirusha maneno yanayodaiwa kumkejeli rais na wananchi, kimepewa onyo kali pamoja na kutakiwa kuomba radhi kwa muda wa siku tatu mfululizo.

“Baada ya kusikiliza na kutafakari kwa kina maelezo ya utetezi yaliyotolewa na Uongozi wa Magic Fm Redio, Kamati ya Maudhui imeridhika kuwa kipindi cha Morning Magic kilikiuka baadhi ya kanuni za huduma za utangazaji 2005. Kamati ya maudhui inaamua kutoa onyo kali kwa Magic Radio, ” alisema na kuongeza.

“Pia inatakiwa kumuomba radhi Rais John Magufuli, wasikilizaji na wananchi kwa ujumla. Tangazo la kuomba radhi litolewe kwa siku tatu mfululizo katika taarifa za habari za saa 10.00 alasriri, na 3.00 usiku kuanzia tarehe 17,9,2016.”

Reviewed by RICH VOICE on Septemba 17, 2016 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...