Marekani: Tutaendelea na mazungumzo na Korea Kaskazini


Waziri wa ulinzi nchini Marekani James Mattis amesema kuwa Marekani itaendelea na mazungumzo ya kidiplomasia na Korea Kaskazini.

Matamshi hayo yanajiri baada ya rais Donald Trump kusema katika mtandao wake wa Twitter kwamba mazungumzo sio suluhu kwa mipango ya kijeshi ya Korea Kaskazini.

Urusi pia imeionya Marekani dhidi ya kuchukua hatua za kijeshi akisema madhara yake yatakuwa makubwa.

Korea Kaskazini ilizua wasiwasi baada ya kurusha kombora kupitia anga ya Japan siku ya Jumanne.

Kombora hilo ambalo Japan limelitaja kuwa tishio lisilo la kawaida , lilivuka katika anga ya kaskazini ya kisiwa cha Japana cha Hokkaido mapema siku ya Jumanne, na kusababisha raia kujificha kabla ya kombora hilo kuanguka baharini yapata kilomita 1,180 .

Korea Kaskzini baadaye ilisema kuwa ni hatua mojawapo ya operesheni zake za kijeshi katika eneo la pacific na kurejelea tishio lake la kushambulia kisiwa cha pacific cha Guam.

Siku chache zilizopita, bwana Trump alikuwa amenukuliwa akisema anaamini kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong un alikuwa ameanza kuiogopa  Marekani.

Lakini katika chapisho lake la siku ya Jumatano , alisema: Marekani imekuwa ikizungumza na Korea Kaskazini na kuwalipa fedha kwa miaka 25.

''Kuzungumza nao sio suluhisho''.lakini alipoulizwa iwapo ni kweli kwamba Marekani imepoteza matumaini ya kidiplomasia , bwana Mattis alitofautiana wazi na rais Trump akisema: Hapana. Sisi hatujapoteza matumaini kupitia kutatua maswala kidiplomasia .

Alikuwa akizungumza alipokutana na mwenzake wa Korea Kusini Song, Young-moo katika Pentagon.

''Tunaendelea kufanya kazi pamoja na waziri na mimi tunagawana majukumu ili kulinda mataifa yetu, idadi yetu na maslahi yetu''
Marekani: Tutaendelea na mazungumzo na Korea Kaskazini Marekani: Tutaendelea na mazungumzo na Korea Kaskazini Reviewed by RICH VOICE on Agosti 31, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...