Watu 9 wakamatwa wakiandamana Posta, Dar es Salaam


Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amethibitisha kukamatwa kwa watu 9 waliokuwa wakiandamana eneo la Samora Avenue, Posta.

Watu hao wamekamatwa baada ya Jeshi la Polisi kuonya kuwa litawachukulia hatua kali wale wote watakaokaidi agizo la kutoandamana kama walivyoagiza.

Watu hao walikuwa wakiandamana kufuatia maandamano yaliyohamasishwa  kupitia mitandao ya kijamii yeye lengo la kupinga baadhi ya mambo yanayofanywa na serikali.

Mbali na watu hao, baadhi ya maeneo mengine ya Jiji la Dar es Salaam leo yamekuwa na watu wachache sana tofauti na siku nyingine za mapumziko, ambapo watu wengi wamekuwa na hofu ya kutoka, kutokana na tetesi za kuwapo kwa maandamano.

Hapa chini ni baadhi ya picha za muonekano wa Jiji la Dar es Salaam;
Watu 9 wakamatwa wakiandamana Posta, Dar es Salaam Watu 9 wakamatwa wakiandamana Posta, Dar es Salaam Reviewed by RICH VOICE on Aprili 27, 2018 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...