Kimbunga Irma chaendelea na uharibifu mkubwa huko Caribbean

This satellite image obtained from the National Oceanic and Atmospheric Administration (NOAA) shows Hurricane Irma at 11:30 GMT on 6 September
Kimbunga Irma kimeelekea visiwa vya Turks na Caicos baada ya kusababisha uharibifu mkubwa huko Caribbean na kuwaua takriban watu 14.
Visiwa vilivyo nyanda za chini vinaripotiwa kuwa kwenye hatari kubwa kukiwa na uwezekano wa kupigwa na mawimbi ya hadi urefu wa mita 6 kuliko viwango vya kawaida.

Kumeripotiwa uharibifu na mafuriko nchini Haiti ambapo miundo mbinu bado ni mibaya tangu litokee tetemeo la ardhi mwaka 2010.
Irma ni kimbunga cha kiwango cha tano.
Hiki ndicho kiwango cha juu zaidi cha kimbunga na upepo wake una kasi ya kilomita 280 kwa saa.

Takiban watu milioni 1.2 wameathiriwa na kimbunga Irma na idadi hiyo huenda ikaongezeka kwa haraka hadi watu milioni 26.
Kuna wasi wasi kuwa ugonjwa unaweza kusambaa kwa haraka maeneo ambapo maji ya kunywa na huduma za usafi zimeathirika, na maafisa wameonya kuwa idadi ya waliokufa huenda ikaongezeka.
Kimbunga hicho kinatarajiwa kufika Cuba baadaye kabla ya kupinga jimbo la Florida huko Marekani mwishoni mwa wiki huku mkuu wa shirika la huduma za dharura la Mareknia akitabiri uharibifu mkubwa.
Maandalizi ya kuwasili kimbunga Irma yalifanywa katika visiwa vya Turks na Caicos ambayo ni himaya ya Uingereza yenye vyenye watu 35,000.
Irma pia kilisababisha uharibifu kwa paa za nyumba na kawi katik sehemu za kaskazini mwa Jamhuri ya Dominica.
Nchini Cuba maelfu ya watalii kutoka maeneo ya kistarehe ya pwani wamehamishwa.
Kimbunga Irma chaendelea na uharibifu mkubwa huko Caribbean Kimbunga Irma chaendelea na uharibifu mkubwa huko Caribbean Reviewed by RICH VOICE on Septemba 08, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...