Anthony Joshua kuvaana na Carlos Takam Oktoba 28

Joshua ameshinda michezo yote 19 aliyocheza

Image captionJoshua ameshinda michezo yote 19 aliyocheza
Bondia Anthony Joshua anatarajiwa kutetea mataji yake ya IBF na WBA atakapovaana na Carlos Takam baada ya Kubrat Pulev kujitoa kufuatia majeraha.
Pambano hilo linalotarajiwa kuwa kali na la kuvutia litapigwa Oktoba 28 katika dimba la Cardiff ambapo mpaka sasa tiyari tiketi 70,000 zimeshauzwa.
Litakuwa pambano la kwanza la Joshua tokea alipomtwanga Wladimir Klitschko katika dimba la Wembley April.
Takam ameshinda michezo 35, amepigwa mitatu na kutoka suluhu mmoja katika mapambano 39 aliyocheza
Image captionTakam ameshinda michezo 35, amepigwa mitatu na kutoka suluhu mmoja katika mapambano 39 aliyocheza
Pulev alipata majereha ya bega wakati akijiandaa na mchezo huo.
Takam mzaliwa wa Cameroon na anayeishi nchini Ufaransa ana miaka 36 na anatarajiwa kutoa upinzani mkali kwa Joshua.
Anthony Joshua kuvaana na Carlos Takam Oktoba 28 Anthony Joshua kuvaana na Carlos Takam Oktoba 28 Reviewed by RICH VOICE on Oktoba 16, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...