Myeshia Johnson: Mjane asema Trump hakukumbuka jina la mumewe


Myeshia Johnson Hollywood, Florida 21 OktobaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMyeshia Johnson akitokwa na machozi akilibusu jeneza la marehemu Hollywood, Florida
Mjane wa mwanajeshi wa Marekani aliyeuawa nchini Niger amesema kuwa alikasiriswa na simu ya pole aliyopigiwa na Rais Donald Trump kwa sababu alionekana kutatizika kulikumbuka jina marehemu mumewe.
Bi Myeshia Johnson mjane wa Sajini La David Johnson ameambia shirika la habari la ABC kwamba kubabaika kwa Rais Trump "kulimuumiza zaidi."
Lakini Bw Trump amejitetea na kusema kwamba alikumbuka na kulitaja jina la Sajini Johnson "bila kusita" na akaeleza mazungumzo kati yake na mjane huyo kwa simu kama ya "heshima sana."
Sajini Johnson aliuawa na wanamgambo wa Kiislamu nchini Niger mwezi huu.
Simu hiyo ya pole ya Trump iligonga vichwa vya habari baada ya mbunge wa Democratic Frederica Wilson aliyeisikiliza pamoja na familia ya mwanajeshi huyo kusema haikuwa na utu.
Myeshia Johnson alionekana kukariri madai ya Bi WIlson kwamba Bw Trump alimwambia mumewe alijua hatari aliyokuwa akijiingiza kwake alipojiunga na jeshi.
Sgt La David JohnsonHaki miliki ya pichaUS ARMY
"Rais alisema alifahamu (Johnson) alikuwa anajiunga na nini, lakini inaumiza...Ilinifanya nilie na kukasirika sana kutokana na alivyoyasema hayo," alisema mjane huyo.
"Alikuwa na ripoti kumhusu mume wangu mbele yake, na hapo ndipo aliposoma La David. Nilimsikia akibabaika akijaribu kulikumbuka jina la mume wangu.
"Iwapo mume wangu alikuwa huko akipigania taifa letu na aliweka maisha yake hatarini kwa ajili ya taifa letu, ni kwa nini hukumbuki jina lake?" aliongeza.
Trump amesemaje?
Rais Trump alijitetea Jumatatu kwenye Twitter na kusema kwamba alitaja jina la mwanajehsi huyo mwanzoni mwa mazungumzo bila kusita.
CHANZO BBC SWAHILI
Myeshia Johnson: Mjane asema Trump hakukumbuka jina la mumewe Myeshia Johnson: Mjane asema Trump hakukumbuka jina la mumewe Reviewed by RICH VOICE on Oktoba 24, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...