Mamake mwanajeshi wa Marekani asema Trump hakuwa na huMamake mwanajeshi wa Marekani asema Trump hakuwa na huruma

Mjane wa mwanajeshi aliyeuawa akibubujikwa na machozi katika jeneza la mumewe

Haki miliki ya pichaCBS
Image captionMjane wa mwanajeshi aliyeuawa akibubujikwa na machozi katika jeneza la mumewe
Rais wa Marekani Donald Trump amejipata mashakani kwa mara nyingine kuhusiana na kauli yake aliyoitoa kwa mjane wa mwanajeshi wa nchi hiyo aliyeuawa vitani nchini Niger.
Rais Trump amekana tuhuma kuwa alimwambia mjane wa mwanajeshi huyo kuwa mumewe alikuwa anajua kile alichoweka saini kwa kazi anayoijua hatma yake.
Mamake mwanajeshi huyo ambaye aliuawa wakati wa vita ameunga mkono madai ya bunge la Congress kwamba rais Trump hakuwa na huruma wakati wa mawasiliano ya simu na mkewe mwanawe marehemu.
Mbunge Federica Wilson alisema kuwa alimwambia Myeshia Johnson : Alijua alichokuwa ametia saini , ''lakini nadhani ni uchungu bila shaka''.
Bwana Trump anasema kuwa madai hayo yalitungwa.
Sajenti La David Johnson aliuawa nchini Niger na wapiganaji wa kiislamu mwezi huu.
Alikuwa mmoja wa wanajeshi maalum waliouawa baada ya kuvamiwa.
Bwana Trump alikuwa tayari amekosolewa kwa kutowasiliana na familia za wanajeshi waliouawa muda mfupi baada ya shambulio hilo la terehe 4 mwezi Oktoba.
Mamake sajenti Johnson , Cowanda Jones-Johnson aliunga mkono kauli ya mbunge Wilson kuhusu mazungumzo hayo ya simu.
Rais Trump hakumuheshimu mwanangu na mkewe pamoja nami na mume wangu , aliambia gazeti la The Washington post.
Donald Trump akiwa Rose Garden ikulu ya White HouseHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionTrump amekanusha tuhuma hizo
Kisa chengine kama hicho kilimlazimu rais Trump kumpatia fedha baba ya mwanajeshi mwengine aliyeuawa akiwa kazini , lakini habari kwamba hakulipa fedha hizo sasa zimejitokeza.
Alisema: Nitakuandikia hundi kutoka katika akaunti yangu binafsi ya $25,000, na nilidanganywa, baba huyo aliliambia gazeti la The Washington Post.
Ikulu ya Whitehouse iliambia gazeti hilo kwamba hundi hiyo ilitumwa na kwamba ilikuwa ishara ukarimu na uaminifu.
Mamake mwanajeshi wa Marekani asema Trump hakuwa na huMamake mwanajeshi wa Marekani asema Trump hakuwa na huruma Mamake mwanajeshi wa Marekani asema Trump hakuwa na huMamake mwanajeshi wa Marekani asema Trump hakuwa na huruma Reviewed by RICH VOICE on Oktoba 19, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...