Messi afunga bao la 100, huku Barcelona ikiilaza Olympiakos


Messi afunga bao la 100, huku Barcelona ikiilaza OlympiakosHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMessi afunga bao la 100, huku Barcelona ikiilaza Olympiakos
Lionel Messi alifunga bao lake la 100 barani Ulaya huku Barcelona ikifanya mechi hiyo kuwa rahisi licha ya kadi nyekundu aliyopewa Gerard Pique na kuilaza Olympiakos katika kombe la vilabu bingwa.
Raia huyo wa Argentina mwenye umri wa miaka 30 alifunga mkwaju wa adhabu na kuwanyamazisha wenyeji wao baada ya mchezaji wa timu hiyo Dimitris Nikolaou kujifunga mapema.
Messi baadaye alimpatia pasi Lucas Digne aliyefunga bao la tatu kabla ya kichwa kizuri cha Nikolaou kupata bao la kufutia machozi.
Pique alipewa kadi ya pili ya njano baada ya kuunawa mpira.
Beki huyo wa kati alitumia mkono wake kuuweka mpira katika eneo hatari baada ya shambulio la Gerard Deulofeu kupanguliwa na kumrudia yeye.
Messi afunga bao la 100, huku Barcelona ikiilaza Olympiakos Messi afunga bao la 100, huku Barcelona ikiilaza Olympiakos Reviewed by RICH VOICE on Oktoba 19, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...