Gari lajeruhi umati wa watu Melbourne, Australia

Polisi wakiokoa majeruhi wa ajali hiyo
Image captionPolisi wakiokoa majeruhi wa ajali hiyo
Gari moja lililokuwa kwenye mwendo wa kasi limewagonga na kuwajeruhi watu kadhaa katika mji wa Melbourne nchini Australia.
Picha kutoka kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha watu wakiwa wameanguka chini, wakitokwa na damu karibu na gari hilo jeupe.
Baadhi ya waliojeruhiwa ni mtoto mdogo ambaye yupo katika hali mbaya.
Polisi inasema bado uchunguzi unaendelea juu ya mtuhumiwa wa tukio hilo
Image captionPolisi inasema bado uchunguzi unaendelea juu ya mtuhumiwa wa tukio hilo
Polisi inasema inaamini kitendo hicho ni cha kukusudia na wanaendelea na uchunguzi.
Dereva wa gari hilo pamoja na mtu mwingine aliyekuwa nae wamekamatwa.
Gari lajeruhi umati wa watu Melbourne, Australia Gari lajeruhi umati wa watu Melbourne, Australia Reviewed by RICH VOICE on Desemba 21, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...