Mahakama nchini Marekani yaruhusu kutekelezwa marufuku ya usafiri ya Trump

trump


Haki miliki ya pichaAFP
Image captionVizuizi vya wageni kutekelezwa

Mahakama kuu nchini Marekani imeamua kuwa toleo la marufuku ya kusafiri ya Rais trump inaweza kutekelezwa kwa ukamilifu.
Huku ikiendelea kukutana na changamoto za kisheria kutoka mahakama za chini.
Nchi sita zinazokutana na zuio hilo ni Iran, Libya, Syria, Yemen, Somalia na Chad.Mahakama za chini tayari zimeruhusu kuzuiwa kwa baadhi ya watu kutoka Korea kaskazini na Venezuela.
Majadiliano Zaidi yatendelea kusikilizwa wiki hii katika mahakama huko San Francisco, California, na Richmond, Virginia.
Mwandishi wa BBC mjini Washington anasema kwamba, kwa sasa, huu ni ushindi mkubwa kwa Donald Trump.
Msemaji wa Ikulu ya White Hogan Gidley alisema kuwa White House haikushangazwa na uamuzi wa mahaka ya juu.
Mwanasheria mkuu Jeff Sessions aliutaja uamuzi huo kama ushindi mkubwa kwa usalama wa watu wa Marekani.
Mahakama nchini Marekani yaruhusu kutekelezwa marufuku ya usafiri ya Trump Mahakama nchini Marekani yaruhusu kutekelezwa marufuku ya usafiri ya Trump Reviewed by RICH VOICE on Desemba 05, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...