Mwimbaji wa Korea Kusini Kim Jong-hyun kuzikwa leo

Kim Jong-hyun alikua mwanamuziki mashuhuri Korea Kusini
Image captionKim Jong-hyun alikua mwanamuziki mashuhuri Korea Kusini
Mazishi ya mwimbaji mashuhuri wa Korea Kusini Kim Jong-hyun, yanafanyika leo hii mjini Seoul.
Mwanamuziki huyo ambaye pia alikua mtangazaji wa radio, mwandishi wa vitabu na mtunzi wa nyimbo, alikutwa amekufa katika tukio linalotajwa kuwa la kujiua.
Umati mkubwa wa watu umekusanyika kumsindikiza katika safari yake ya mwisho, huku mwili wake ukibebwa na gari aina ya limousine nyeusi kutoka hospitalini alipohifadhiwa kwa takriban siku tatu.
Picha yake iliwekwa hospital mjini Seoul
Image captionPicha yake iliwekwa hospital mjini Seoul
Ibada ya kumuaga kifamilia ilifanyika mapema pia mjini Seoul.
Mwanamuziki huyo aliyekua na miaka 27 akiimbia bendi ya Shinee,alikutwa ameanguka kutoka ghorofa moja refu la kupangisha siku ya Jumatatu.
Mwimbaji wa Korea Kusini Kim Jong-hyun kuzikwa leo Mwimbaji wa Korea Kusini Kim Jong-hyun kuzikwa leo Reviewed by RICH VOICE on Desemba 21, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...