BREAKING NEWSSSSSSSSSSSSS:Rais Robert Mugabe amejiuzulu

Rais Robert Mugabe amejiuzulu
Image captionRais Robert Mugabe amejiuzulu
Katika dakika chache zilizopita , spika wa bung la Zimbabwe ametangaza kuwa rais Robert Mugabe amejiuzulu .
Spika wa bunge Jacob Mudenda alisema kuwa hatua hiyo ni ya kujitolea na amefanya hivyo ili kuweza kuwepo kwa mabadiliko mazuri ya mamlaka kulingana na chombo cha habri cha reuters.
Tangazo hilo la ghafla lilizuia harakati za bunge kutaka kumng'oa madarakani ambazo zilikuwa zimeanza dhidi yake.
Kwa mujibu wa chombo cha habari cha Reuters, Spika wa bunge amesema kuwa kiongozi mpya atawekwa madarakani siku ya kesho Jumatano.
Wabunge walifurahia kufuatia hatua hiyo na raia wameanza kusherehekea barabarani.
Awali bwana Mugabe alikuwa amekataa kujiuzulu licha ya jeshi kuchukua mamlaka huku hatua hiyo ikifuatiwa na maadamano ya raia waliotaka kiongozi huyo kung'atuka mamlakani wiki hii.
BREAKING NEWSSSSSSSSSSSSS:Rais Robert Mugabe amejiuzulu BREAKING NEWSSSSSSSSSSSSS:Rais Robert Mugabe amejiuzulu Reviewed by RICH VOICE on Novemba 21, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...