Tetemeko nchini Iran na Iraq lawaua zaidi ya watu 348

A damaged storefront is seen after an earthquake in Halabja, Iraq

Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionTetemeko nchini Iran na Iraq lawaua zaidi ya watu 200
Tetemeko la ukubwa wa 7.3 katika vipimo vya richa limekumba eneo la kaskazini mwa Iran na Iraq na kuua watu kadha.
Takriban watu 348 waliuawa katika mkoa ulio magharibi mwa Iran wa Kermanshah, kwa mujibu wa maafisa.
Tetemeko hilo lilizua hofu hadi kusababisha watu kukimbia kutoka manyumbani mwao kwenda barabarani.
Misikiti kwenye mji mkuu wa Iraq Baghdad, imekuwa ikifanya maombi kwa kutumia vipasa sauti.
Wengi wa waathiriwa walikuwa ni kwenye mji wa Sarpol-e Zahab, kilomita 15 kutoka mpakani.
Kulingana na kituo cha Marekani USGS tetekemo hilo lilitokea umbali wa kilomita 33.9 chini ya ardhi la lilisikika nchini Uturuki, Israel na Kuwait
Three Baghdad residents in the streets after a powerful earthquake struck
Image captionTetemeko nchini Iran na Iraq lawaua zaidi ya watu 200
Uharibifu umeripotiwa kuetka katika vijiji vinane kwa mujibu wa shirika la msalaba mwekundu nchini Iran Morteza Salim.
Baadhi ya vijiji vimekumbwa na matatizo ya nguvu za umeme na mawasiliano yamevurugwa
Makundi ya uokoaji yanatatizwa na maporomoa ya ardhi.
Tetemo hilo lilitokea kilimita 30 kusini magharibi mwa mji wa Halabja karibu na mpaka wa Iran.
Lilitokea umbali wa kilomita 33.9 na lilisikika nchini Uturuki, Israel na Kuwait.
CHANZO:BBC SWAHILI
Tetemeko nchini Iran na Iraq lawaua zaidi ya watu 348 Tetemeko nchini Iran na Iraq lawaua zaidi ya watu 348 Reviewed by RICH VOICE on Novemba 13, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...