Watalii wa Marekani wakamatwa kwa kuonyesha makalio hekaluni Thailand

Watalii wa Marekani wakamatwa kwa kupiga picha za utupu hekaluni

Haki miliki ya pichaINSTAGRAM
Image captionWatalii wa Marekani wakamatwa kwa kupiga picha za utupu hekaluni
Raia wawili wa Marekani wamekamatwa nchini Thailand baada ya kuchapisha picha yao mtandaoni wakionyesha makalio yao katika hekalu.
Watalii hao walipiga picha hiyo katika hekalu maarufu nchini Bangkok Wat Arun na kuichapisha katika mitandao ya Twitter na instagram.
Mamlaka ya uhamiaji iliambia BBC kwamba wawili hao Joseph na Travis Dasilva wote wakiwa na umnri wa miaka 38 watapigwa faini na kurudishwa kwao.
Thailand ina sheria kali kuhusu tabia zinazoonekana kutokuwa na heshima na zinazoingilia dini yake ya Buddha.
Watalii hao walikamatwa jioni Jumane wakati walipokuwa wakiondoka nchini humo katika uwanja wa ndege wa Bankok Don Mueang.
Naibu msemaji wa idara ya uhamiaji nchini Thailand, kanali Choengron Rimpadee aliambia BBC kwamba wawili hao walikuwa katika orodha ya watu waliokuwa wakichunguzwa baada ya mamlaka kuona picha hizo zenye utata katika mitandao ya kijamii.
''Wakati watakaposhtakiwa maafisa wa polisi wa uhamiaji wa Thailand watafutilia mbali visa zao na kutaka warudishwe makwao'', alisema.
Watalii wa Marekani wakamatwa kwa kupiga picha za utupu hekaluni ThailandHaki miliki ya pichaTHAI IMMMIGRATION POLICE
Image captionWatalii wa Marekani wakamatwa kwa kupiga picha za utupu hekaluni Thailand
Pia watapigwa marufuku kurudi nchini Thailand.
Alielezea kwamba wawili hao waliwasilishwa katika kituo cha polisi cha Yai nchini Bangkok ili kushtakiwa kwa kuonyesha utupu katika eneo la umma, makosa ambayo mtu anapopatikana na hatia anaweza kupigwa faini ya dola 153.
Hatahivyo, serikali ya Thai na maafisa wa polisi wameambia vyombo vya habari kwamba mashtaka hayo yanaweza kuwa mabaya zaidi.
Watalii wa Marekani wakamatwa kwa kuonyesha makalio hekaluni Thailand Watalii wa Marekani wakamatwa kwa kuonyesha makalio hekaluni Thailand Reviewed by RICH VOICE on Novemba 30, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...