Polisi wavamia wahamiaji Papua New Guinea

Mamlaka zikiwaondosha wanaoomba uhamiaji Papua New Guinea

Haki miliki ya pichaAFP PHOTO / GETUP
Image captionMaafisa wa Papua New Guinea walikuwa wamewapatia wahamiaji muda wa kuondoka.
Polisi wa Papua New Guinea (PNG) wameingia katika kituo cha mahabusu cha wahamiaji kilichokuwa kinamilikiwa na Australian kwa azma ya kuwaondosha wanaoomba uhamiaji waliosalia, imethibitisha serikali ya Australia.
Mamia ya wanaume wamekataa kuondoka kwenye kituo hicho kilichopo katika kisiwa cha Manustangu kilipofungwa tarehe 31 Oktoba, wakielezea hofu ya usalama wao.
Alhamisi, wanaume waliokuwa katika kituo hicho walisema polisi wa PNG walikuwa wamewapatia saa moja wawe wameondoka.
Australia imesema kuwa operesheni hiyo inaendeshwa na Papua New Guine- PNG.
Chini ya sera tata, Australia iliwashikilia watu wanaoomba uhamiaji wanaowasili kwa boti kwenye kambi katika visiwa cha Manus na Nauru, ambalo ni taifa dogo leneo la Pacific.
Image copyrightABDUL AZIZ ADAM
Uharibifu wa vifaa katika kituo cha wahamiajiHaki miliki ya pichaABDUL AZIZ ADAM
Image captionMahabusu wa zamani anasema maafisa wameharibu vifaa kwatika kito cha kuwahifadhi wahamiaji
Australia ilifunga kituo hicho cha kisiwa cha Manus baada ya mahakama ya PNG kuamua kuwa kilikuwa ni kinyume cha sheria, na kuwataka wanaoomba uhamiaji kuhamia kwenye vituo vingine vya wanaoomba uhamiaji vilivyopo kwenye maeneo mengine ya kisiwa hicho.
Waziri mkuu wa Australia Malcolm Turnbull alisema kuwa taifa lake ''halitashinikizwa " kuwakubali wanaume hao wahamiaji, akirejelea kuwa sera ya muda mrefu ya kuwashikilia itachochea biashara haramu ya binadamu.
" Wanapaswa kuheshimu sheria na mamlaka za kisheria za Papua New Guinea,"Alisema waziri mkuu wa Australia Bwana Turnbull.
Mmoja wa wakimbizi hao, Abdul Aziz Adam, alisema kwua watu wapatao 420 wanaoomba uhamiaji walibakia kwenye kituo hicho Alhamis Thursday, na walikuwa watulivu.
Watu hao walikataa kuondoka kwasababu wanahofia kuwa wanaweza kushambuliwa na jamii za watu waishio kwenye kisiwa hicho.
Makundi ya kutete haki za binadamu yansema wahamiaji hao wamewahi kushambuliwa awali.
Polisi wavamia wahamiaji Papua New Guinea Polisi wavamia wahamiaji Papua New Guinea Reviewed by RICH VOICE on Novemba 23, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni

Chapisho Lililoangaziwa

Thursday, September 15, 2016 Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Septemba 15 ...